Cibitoke : Zaidi ya familia 100 walifukuzwa nje ya ardhi zao eneo la Rugombo
Karibu familia mia moja kwenye kitongoji cha Mbaza-Miduha kijiji cha Rukana ya pili tarafani Rugombo katika mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi) wanasema kuwa walinyanganywa ardhi zao. Wanawanyoshea kidole na kuwatuhumu viongozi tawala katika mkoa huo kuwa waliahidi kupatia ardhi hizo vigogo wafuasi wa chama cha CNDD-FDD. Gavana wa mkoa anakiri ardhi hizo ni miliki ya a serikali. HABARI ya SOS Medias Burundi
Takriban familia 110 zilizokuwa kwenye ardhi yenye ukubwa wa heka 80 wamefurushwa nje ya ardhi yao kwenye kitongoji cha Mbaza-Miduha.
Kulingana na vyanzo vya habari sehemu hiyo, vijana Imbonerakure ( wafuasi wa chama tawala cha CNDD-FDD) walimiminika wakiwa idadi kubwa tangu wiki moja na kuwalazimisha jumla ya wakaazi wa eneo hilo kuondoka mara moja bila masharti.
“Vijana hao walituambia kuwa tunaishi katika ardhi zinazomilikiwa na serikali na kwamba hatuna haki yoyote za kuendelea tukiishi eneo hilo” ameeleza mkaazi mmoja aliyekutwa sehemu hiyo.
Kulingana na wakaazi, ” ni hali ya kupokonywa ardhi kwa manfaa ya ummaa. Ardhi hiyo zimechukuliwa na kupewa vigogo raia na wanajeshi wafuasi wa chama cha CNDD-FDD”.
Chanzo katika watu wakuu kinafahamisha kuwa zaidi ya heka 100 za ardhi eneo hilo zilikabidhiwa watu wa karibu na CNDD-FDD mwanzoni mwa mwaka huu.
Baadhi ya wakaazi wa Mbaza-Miduha wanaishi eneo hilo kwa zaidi ya karne moja.Wengine walikabidhiwa ardhi kisheria na wako na karatasi za umuliki wa ardhi. Familia zilizopokonywa ardhi hizo upande wao wanawaomba viongozi wanaohusika “Kuheshimisha haki yao kwenye ardhi za ma babu zao”.
Gavana wa mkoa wa Cibitoke anakiri kuwa ardhi hiyo ya Mbaza-Miduha ni mali ya serikali na kwamba serikali inachukuwa mali yake. Ama kuhusu swali kwamba ardhi hizo zinakabidhiwa kwa watu wa karibu na chama tawala na kwa baadhi ya wafanyakazi wa ummaa baada ya kunyanganywa wakaazi, Carême Bizoza amejizua kusema lolote.
You might also like
Photo of the week-Uganda : towards the ban on the beating of Burundian drums among refugees
The Burundi Embassy in Kampala, Uganda has issued a memorandum prohibiting the beating of drums anywhere in Uganda. It also called on cultural clubs to hand over their drums to
Cibitoke: the governor bans the sale of corn outside the province
The Cibitoke provincial authority (north-west Burundi) took a decision seen as controversial as it bans the sale of maize outside the province. Farmers decribe it as unjust because it deprives
Ngozi: lack of food ration at the main prison
Detainees, in the main prison of Ngozi (northern Burundi) have no food. The most affected are those from the provinces of Kirundo and Kayanza (same region) who expect any interventions
