Tanzania : zaidi ya wakimbizi 4750 wa burundi wamekamatwa kwa kipindi cha miezi minne wakijaribu kwenda katika za ukanda huu
Takwimu hizo zilitolewa na huduma ya uhamiaji katika tarafa ya Kakonko, kanda ya kigoma (kaskazini-magharibi mwa Tanzania) ambako wahusika wanapitia. Ilikuwa alhamisi hii. Kulingana na ushuhuda wa wakimbizi, wanataka kukimbia kambi nchini Tanzania kutokana na hali mbaya ya maisha. Hakika ni karibu 4750 wanaohusishwa. HABARI ya SOS Medias Burundi
Kulingana na viongozi nchini Tanzania, ni wakuu wa familia changa pamoja na wale wanaowategemea ambao kubwa wanakamatwa katika visa vingi.
” Ni rahisi kwao kutumia usafiri wa watu na vitu ukilinganisha na takaba zingine za wakimbizi. Na hilo kwa safari ndefu” vyanzo vyetu zinadai.
Wakimbizi wa burundi waliokamatwa walitaka kuelekea nchini Rwanda, Uganda, na Kenya kwa mjibu wa huduma ya uhamiaji eneo la Kakonko.
” Tunakabiliana na hali ngumu ya maisha ndani ya kambi.Msaada wa chakula hautoshi na shughuzi za kuleta faida zilisimamishwa. Tunapata pia ugumu kutoka ili kwenda kulima katika mashamba ya watanzania au katika vijiji vya karibu. Hali inaendelea kuwa ngumu kwetu ndio maana tunataka kwenda sehemu nyingine. Cha ajabu ni kwamba wanataka kuturejesha nyumbani kwa nguvu “, wamefafanua kwa polisi ya tanzania warundi waliokamatwa eneo la Kakonko.
Kakonko tarafa ambako kunapatikana kambi ya Mtendeli iliyofungwa hivi karibuni inasalia eneo peke la mpaka ambako warundi wanaokimbia kambi huwa wanalazimika kupita ili kuwasiki katika nchi za kanda hii wanakotaka kufika.
Kwa mjibu wa wandishi wetu ndani ya kambi za wakimbizi wa burundi nchini Tanzania, wakimbizi kwa sasa hawaripoti kwa wingi zoezi la kurejeshsa nchini kwa hiari katika miezi ya nyuma. Hali hii inawapelekea viongozi wa Tanzania kudumaza hali ya maisha ndani ya kambi.
Tanzania inasalia kuwa nchini ya kwanza inayopokea wakimbizi kutoka burundi. Inawapa hifadhi takriban laki moja na elfu 27 ambao wako katika kambi mbili ambazo ni Nduta na Nyarugusu katika mkoa wa Kigoma kaskazini-magharibi mwa nchi.
You might also like
Tanzania: viongozi watawafukuza tena wakimbizi wa zamani wa burundi waliorudi uhamishoni
Kwa jumla, ni raia wa burundi 1048 wanaolengwa na hatua hiyo. Wote ni wakimbizi wa zamani waliorudi ukimbizini katika miaka miwili iliyopita baada ya kurudi nchini Burundi. Walengwa hao wanaomba
Mahama (Rwanda) : repetitive shortage of cooking gas stocks
Refugees from the Mahama camp in Rwanda denounce a cycle of shortages of cooking gas stocks. They are at least two weeks behind schedule each month, which aggravates the situation
Nyarugusu (Tanzania) : a hospital closed, Burundian refugees contact the UNHCR
SOS Médias Burundi Nyarugusu, September 11, 2025 – The NGO Medical Team International has closed one of its hospitals in the Nyarugusu refugee camp in Tanzania, a decision that has
