Mwanamfalme Louis Rwagasore: Hospitali inayoumwa zaidi ya wagonjwa inayowapokea
Tangu kuanzishwa mwaka 1945, cliniki ya Prince Louis Rwagasore ilitoa huduma kwa wagonjwa mashuhuri na watu wa kipato cha juu wa wakati wa ukoloni na baadaye. Ilipendwa na kuendelea kupendwa kutokana na mfumo wake wa ujenzi wa kikoloni lakini jengo hilo limechakarika na liko katika hatari ya kubomoka kutokana na kutoshughulikiwa. HABARI ya SOS Medias Burundi
Kliniki ya Prince Louis Rwagasore iliyojengwa kati kati mwa jiji la Bujumbura makao makuu ya kiuchumi, sasa ni jengo lililochakarika. Ni kituo cha afya cha watu wenye kipato cha chini waliothubutu kwenda kutafuta huduma zinazolingana na uwezo wao mdogo.
Kituo hicho cha afya hakiaminiki. Watu wanakwenda kujitibisha lakini kwa maoni ya wagonjwa wenye uelewa, ni rahisi sana kupata kifo.
Manesi kwenye hospitali hiyo ya zamani kabisa ndani ya nchi ndogo ya afrika mashariki wanasema hakuna kinachoendelea.
“Tuko na tatizo la dawa. Kutokana na uhaba wa dawa, hatuwezi kutoa huduma hasa katika kipindi hichi cha majanga. Kuna tatizo ya vifaa : Kwenye maabara, chumba cha upasuaji, ndani ya huduma zote. Vifaa vimeharibika. Tunashudia mara kwa mara matatizo” alisema nesi mmoja aliyefanya miaka 29 ya kazi kwenye kliniki ya Prince Louis Rwagasore.
“Kuhusu hospitali hiyo, tuna matatizo kabisa. Mara nyingi unaweza kuwa na afya nzuri, lakini unapokwenda kwenye kliniki ya Prince Louis Rwagasore, utapata maradhi. Vyote vimechafuka, vyoo ….mbu wanakung’ata”, anahakikisha Hervé mgonjwa aliyekutwa kwenye mapokezi.
Kama aliyeshuhudia mmoja kati ya ma ripoti wetu, panya wanakula michafu ya hospitali hiyo iliyowekwa ndani ya ndoo ambazo ziko wazi.
“Tuna matatizo ya kihistoria ya uhaba wa wafanyakazi, madaktari bingwa na madawa na isitoshi kuna rushwa na matumizi mabaya ya bajeti. Huduma za afya zinakabiliwa na matatizo kwa kipindi cha miaka tisa hadi sasa.” alibaini mganga wa magonjwa ya wanawake kwenye hospitali hiyo ambaye hakutaka jina lake litambulike.
Kwa mjibu wa mganga mkuu wa kliniki hiyo jawabu liko katika mikono la serikali.
“Ili huduma za hospitali ziendeshwe, ni lazima bajeti ipatikane. Ni miaka mingi tukiomba bajeti kwa serikali ili tuendeshe hospitali hiyo ya umaa lakini tunapata moja kwa kumi tunazoomba, ni kawaida huduma za hospitali kutokuwa vizuri” alifahamisha Dk Bonith Havyarimana mganga mkuu wa kliniki ya Prince Louis Rwagasore.
You might also like
Photo of the week : at least 16 people bitten by stray dogs in Kayanza
At least 16 people from the districts of Kayanza, Gatara and Muruta in Kayanza province (northern Burundi) have been bitten by stray dogs. The population speaks of panic “especially since
Burundi : kitita cha milioni 21 chatolewa na benki ya afrika ya maendeleo kwa ajili ya kuendeleza sekta ya kilimo
Mikoa ya kaskazini mashariki mwa Burundi ambayo ni : Ngozi, Kirundo na Muyinga itanufaika na mradi hui kwa kutengeneza mabonde ya mito mingi. Lengo ni kuongeza mavuno ya kilimo kwa
Ciibitoke : a farmer brutally beaten to death in a disputed field
SOS Médias Burundi, Cibitoke, – The lifeless body of Julienne Nahayo, 59 years old, was discovered Sunday afternoon in a cassava field in Gabiro-Ruvyagira village, in the Rugombo zone, Cibitoke
