Karusi-Rumonge: mikoa hiyo imewapata magavana wapya
Léonard Niyonsaba na Dévote Nizigiyimana, wa kwanza ni gavana mpya wa mkoa wa Rumonge (Kusini-magharibi mwa Burundi) na mwingine ni gavana wa mkoa wa Karusi (Mashariki ya kati mwa Burundi). Waliidhinishwa na baraza la seneti siku ya jumatano baada ya majina yao kupendelezwa na rais wa jamuhuri. Wakaazi wa mkoa wa Rumonge wanasema kuridhishwa na mabadiliko hayo ya kiongozi wa mkoa. Gavana huyo anayeondoka ameacha mkoa huo ukiwa masikini licha ya fursa nyingi zilizopo, ikiwa ya mwisho nchini katika rikodi ya elimu na kwingine. Wakaazi wa mkoa huo wanaomba kiongozi mpya kuunganisha wananchi waliotenganisha wa gavana aliyesimamishwa. HABARI SOS Médias Burundi
Léonard Niyonsaba ambaye ameteuliwa kuwa gavana mpya wa mkoa wa Rumonge, hadi sasa alikuwa mkuu wa itifaki katika ofisi ya gavana aliyeachishwa ngazi Consolateur Nitunga. Huyu naye aliteuliwa kuwa mshahuri wa pili kwenye ubalozi wa Burundi nchini DRC.
Mkoa mwingine uliopata kiongozi mpya ni Karusi. Ni Dévote Nizigiyimana. Yeye alikuwa mfanyakazi kwenye ENS ( Chuo cha waalimu).
Mkoani Rumonge, wakaazi wanalaani kuona Consolateur Nitunga ameacha mkoa ambao haujaweza kunufaika na fursa zilizopo katika mkoa huo.
” Alijulikana katika visa vya rushwa kuliko kupendelea mzunguko wa biashara. Hatua ya kuruhusu bidhaa za nafaka kuingia tena nchini Burundi haikuleta matunda. Bei ya kilo moja ya mchele ni hadi 3600 sarafu za Burundi kwa mfano wakati ambapo tuko na bandari ambako kunapita bidhaa kwa urahisi, [….], wanalalamika wakaazi huku wakikumbusha kuwa rais Ndayishimiye alimuaibisha gavana huyo aliyeondolewa katika mwezi juni kutokana na visa vya ulaji rushwa kuhusu mafuta ya gari na theluji. Kuna mshahuri ya gavana wa mkoa wa Rumonge aliyefutwa kazi kwa hoja hizo hizo mwezi huu.
Waangalizi maeneo hayo wanahofu kuwa gavana mpya atakuwa na kibarua kigumu cha kuunganisha wananchi waliotofautishwa na mtangulizi wake sababu ” alifanya kile chote anachoweza ili kutofautisha watu kwa misingi ya ukabila. Ana ukabila mwingi na chuki dhidi ya Watutsi na wapinzani wote wa kisiasa”.
Rumonge ni kati ya mikoa ambayo iko na fursa nyingi. Mkoa huo unapatikana kwenye mwambao wa ziwa Tanganyika na unazalisha kwa wingi Mafuta ya migazi inayotumiwa katika nchi hii ndogo ya afrika mashariki na nchi jirani pamoja pia uzalishaji wa matunda.
You might also like
Rumonge : the government regrets the enormous expenses incurred in prisons
The Vice-President of the Republic of Burundi, Prosper Bazombanza expressed the regrets of the government which plans to spend this year around 15 billion Burundi francs from its general budget
Rumonge : the government adopts an additional envelope of 18 billion for rehabilitation works of the RN3
The Council of Ministers adopted this week an envelope of eighteen billion additional francs for the rehabilitation project of the national road number three (RN3). The government spokesperson indicates that
Cibitoke: general increase in the prices of basic necessities
A generalized spike in stuff price is observed across the communes of Cibitoke province (north-west Burundi) with people asking the government to fix the matter. The governor warns speculators saying
