Giharo: mjumbe wa chama cha CNDD-FDD mwenye ushawishi anazuiliwa jela
Nestor Butisi, mjumbe wa chama tawala tarafani Giharo mkoa wa Rutana (Kusini mashariki mwa Burundi) amesimamishwa jumatatu iliyopita. Anatuhumiwa kufanya biashara haramu ya mbolea na kutengeneza pombe haramu. Anazuiliwa katika gereza la mkoa. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na wakaazi wa tarafa ya Giharo, ni polisi waliomusimamisha baada ya msako kufanyika nyumbani kwako.
Polisi iligundua nyumbani kwake mifuko 35 ya mbolea ya kizungu, mifuko 17 ya sukari na jerikani 9 za pombe iliyopigwa marufuku.
Mfuasi huyo wa chama cha CNDD-FDD mwenye ushawishi alishikiliwa katika gereza la kamishena ya polisi tarafa Giharo kwa masaa 24.
Alichukuliwa na Mwendeshamashtaka wa jamuhuri mkoani Rutana siku moja baada ya kukamatwa na kutumwa katika gereza la mkoa alhamisi iliyopita nyakati za alasiri.
Vyanzo katika chama tawala vinasema kuwa katibu mkuu wa chama cha CNDD-FDD tarafani Giharo alifanikiwa kumuelewesha mwendeshamashtaka ili kesi isiwe ya mafumanio kwa kosa ” biashara haramu ya mbolea ” sawa na matakwa ya serikali kuhusiana na kupiga vita biashara haramu ya mbolea.
Fundi wa kilimo mmoja pia mfuasi wa chama tawala alisimamishwa mwaka jana kwa tuhuma za wizi wa tani nyingi za mbolea. Hakumaliza muda mrefu katika gereza la korti ya Rutana. Aliachiliwa kwa ushawishi wa kiongozi wa chama cha CNDD-FDD.
Bwana Butisi alitajwa katika visa vingi vya kuwahujumu wapinzani mkoani Rutana ikiwa ni pamoja na visa vya kukamatwa kinyume cha sheria.
You might also like
Nyanza-Lac: the communal administrator and all his aids sacked
Marie Goreth Irankunda, communal administrator of Nyanza-Lac (province of Makamba, southern Burundi) as well as Prudence Kabura and Elias Ciza respectively president and vice-president of the communal council were dismissed
DRC-EAC: en route to the establishment of a monitoring and verification mechanism in eastern DRC
The East African community plans to send a monitoring and verification mechanism to eastern DRC, a mécanism so crucial to end conflicts, said a press release published on the EAC
Aloys Baricako (RANAC) accuses generals of hijacking the state and promises a national reconstruction
SOS Médias Burundi Gitega, June 2, 2025 — In Gitega, Aloys Baricako is breaking his silence. The RANAC president openly accuses certain generals and senior officials of misappropriating public resources
