Giharo: mjumbe wa chama cha CNDD-FDD mwenye ushawishi anazuiliwa jela
Nestor Butisi, mjumbe wa chama tawala tarafani Giharo mkoa wa Rutana (Kusini mashariki mwa Burundi) amesimamishwa jumatatu iliyopita. Anatuhumiwa kufanya biashara haramu ya mbolea na kutengeneza pombe haramu. Anazuiliwa katika gereza la mkoa. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na wakaazi wa tarafa ya Giharo, ni polisi waliomusimamisha baada ya msako kufanyika nyumbani kwako.
Polisi iligundua nyumbani kwake mifuko 35 ya mbolea ya kizungu, mifuko 17 ya sukari na jerikani 9 za pombe iliyopigwa marufuku.
Mfuasi huyo wa chama cha CNDD-FDD mwenye ushawishi alishikiliwa katika gereza la kamishena ya polisi tarafa Giharo kwa masaa 24.
Alichukuliwa na Mwendeshamashtaka wa jamuhuri mkoani Rutana siku moja baada ya kukamatwa na kutumwa katika gereza la mkoa alhamisi iliyopita nyakati za alasiri.
Vyanzo katika chama tawala vinasema kuwa katibu mkuu wa chama cha CNDD-FDD tarafani Giharo alifanikiwa kumuelewesha mwendeshamashtaka ili kesi isiwe ya mafumanio kwa kosa ” biashara haramu ya mbolea ” sawa na matakwa ya serikali kuhusiana na kupiga vita biashara haramu ya mbolea.
Fundi wa kilimo mmoja pia mfuasi wa chama tawala alisimamishwa mwaka jana kwa tuhuma za wizi wa tani nyingi za mbolea. Hakumaliza muda mrefu katika gereza la korti ya Rutana. Aliachiliwa kwa ushawishi wa kiongozi wa chama cha CNDD-FDD.
Bwana Butisi alitajwa katika visa vingi vya kuwahujumu wapinzani mkoani Rutana ikiwa ni pamoja na visa vya kukamatwa kinyume cha sheria.
You might also like
Elections in Burundi : journalists struggle to leave Bujumbura to cover the vote
SOS Médias Burundi Bujumbura, June 4, 2025 – On Wednesday evening, on the eve of the legislative and district elections scheduled for Thursday, June 5, 2025, several Burundian journalists remained
DRC: kiongozi wa zamani wa waasi Jean Bosco Ntaganda ametumwa katika jela nchini ubelgiji
Kulingana na mkataba wa mahakama ya kimataifa, mahabusu waliokatiwa kesi wanalazimika kutumikia kifungo chao katika nchi iliosaini mkataba wa Roma juu ya uundwaji wa ICC. Jean Bosco Ntaganda kiongozi wa
Nyanza-Lac: a former village chief beaten up by an Imbonerakure
Patrice Ntiganzwa, former chief of Muyange vill in Nyanza-Lac district, Makamba province (southern Burundi) was seriously beaten up by an Imbonerakure (CNDD-FDD party youth league member) on Sunday night. The
