Rutana: mfuasi mwenye ushawishi wa chama cha CNDD-FDD akungwa mwaka mmoja jela
Nestor Butisi Nibigira mfanyabiashara na mfuasi mwenye ushawishi wa chama cha CNDD-FDD tarafani Giharo amekatiwa kifungo cha mwaka mmoja jela. Atalazimika kulipa faini ya milioni 2.5 sarafu za burundi. Uamzi umechukuliwa jumatano hii alasiri baada ya kesi dhidi yake asubuhi ya hiyo siku katika korti ya Rutana (Kusini mashariki mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi
Mtuhumiwa aliripoti mbele ya jopo la majaji wa korti ya mkoa wa Rutana jumatatu ambalo limeamuru asalie gerezani.
” Kesi dhidi yake, iliharakishwa zaidi ya kesi za wafungwa wengine”, chanzo kwenye korti ya Rutana kinahakikisha.
Katika siku mbili peke, aliripoti mbele ya jopo la majaji na kesi yake kusikilizwa. Maanuzi yalichukuliwa siku hiyo hiyo.
“Vigogo wa chama cha CNDD-FDD waliwashawishi majaji , waliwapa maelekezo ” , chanzo karibu na faili hiyo kinaeleza.
Nestor Butisi Nibigira alikuwa alisimamishwa na polisi baada ya msako wa tarehe 24 oktoba. Mifuko 35 ya mbolea ya kizungu, 17 ya sukari na jerikani 9 za pombe haramu vilikamatwa kwenye duka lake na nyumbani kwake.
Mfuasi huyo na mwenye ushawishi wa chama tawala anafahamika katika tarafa ya Giharo kama mtu aliyeshiriki katika kamata kamata ya kiholela ya wa upinzani hasa wafuasi wa chama cha CNL.
Kosa peke la ubadilifu na biashara haramu ndilo lilizingatiwa dhidi yake.
You might also like
Burundi : social unrest over the high cost of living, tensions between workers and the government amid economic constraints
SOS Médias Burundi Gitega, May 1, 2026 – The celebration of the International Workers’ Day, held on Friday at the Ingoma Stadium in Gitega, the political capital of the small
Bujumbura : chama cha CNL chazuiliwa kuadhimisha kumbukumbu ya miaka minne
Waziri wa mambo ya ndani na usalama aliamuru kupiga marufuku sherehe za maadhimisho ya miaka minne ya uhai wa chama cha CNL na zile za kutakiana rheli za mwaka mpya
Burunga : CEPI accused of authoritarian drift, the opposition denounces CNDD-FDD takeover
SOS Médias Burundi Burunga, May 13, 2025 – With just two months to go before the elections, the Burundian opposition is sounding the alarm. In Burunga province (southern Burundi), political
