Nyabihanga : Imbonerakure wawili gerezani
Emmanuel Ndimurirwo na César Sinduhijimana wanazuwiliwa katika gereza la kamishena ya polisi ya mkoa wa Mwaro (kati kati mwa Burundi) tangu jumatano wiki iliyopita. Wawili hao ni wenye asili ya tarafa ya Nyabihanga (katika mkoa huo huo), wanatuhumiwa wizi na unyanyasaji. HABARI SOS Médias Burundi
Ni Emmanuel Ndimurirwo maarufu l’homme ambaye huenda alibaka mtoto wa kike mkaazi wa kijiji cha Miterama tarafa ya Nyabihanga. Kwa mjibu wa vyanzo eneo, hali ilikwenda vibaya baada ya ukatili huo.
Baada ya siku kadhaa, mtuhumiwa huyo wa ubakaji alijikuta akiwa hana tena nguvu ya kufanya kitendo cha ndoa na mke wake, vyanzo vya karibu na faili hiyo vinadai ni kutokana na ” uchawi”.
Alitafuta uungwaji mkono kutoka kwa afisa wa idara ya ujasusi tarafani Nyabihanga pamoja na César Sinduhijimana ambaye ni kiongozi wa tawi la Imbonerakure wafuasi wa chama cha CNDD-FDD.
” Malengo yake ilikuwa kumutisha mtoto huyo wa kike ili amutibu Emmanuel”, kwa mjibu wa vyanzo vyetu.
” Wanaume hao walimutishia wakiwa na visu mkononi, na mtoto huyo wa kike akakubali kulala mara mbili na Emmanuel “.
Wazazi wa mtoto huyo walitoa mashtaka na wanaume hao wote watatu walikamatwa na kupelekwa kwenye kamishena ya polisi ya Mwaro.
Mkuu wa idara ya ujasusi wa Mwaro aliachiwa huru siku chache badaye.
Emmanuel Ndimurirwo ni mwalimu. César Sinduhijimana yeye ni kiongozi wa shule ya msingi.
Familia ya muhanga inaomba ” mtoto wao apewe ulinzi”. Familia hiyo inaomba uchunguzi huru ufanyike.
Kisa ambapo kinafanya wanaume hao wawili kufuatiliwa, kilifanyika wiki mbili zilizopita.
You might also like
Masisi: the M23 progressing towards Sake city
Violent clashes between the FARDC (DRC armed forces) and the M23 armed group are happening in Masisi territory, in the province of North Kivu in eastern Congo. The DR troops
Photo of the week – Bubanza : former MP Fabien Banciryanino sparks controversy
On the occasion of the commemoration of the assassination of President Melchior Ndadaye, former deputy Fabien Banciryanino brought a flower on which is inscribed that the democracy that Ndadaye advocated
Goma: wandishi wa habari kusimamishwa wakati wakiripoti juu ya mandamano dhidi ya kikosi cha EAC
Hali ya taharuki imeripotiwa katika mji wa Goma mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC kufuatia mandamano dhidi ya kikosi cha EAC jumatano hii. Askali polisi pamoja na wanajeshi wametumia
