Goma: mwandishi wa habari azuiliwa na idara ya ujasusi

Goma: mwandishi wa habari azuiliwa na idara ya ujasusi

Jimmy Shukrani Bakomera mwandishi wa habari na ripota wa VOA (Sauti ya Amerika) Kirundi-Kinyarwanda anazuiliwa na idara ya ujasusi ya Kongo tangu alhamisi hii. HABARI SOS Médias Burundi

Mwenzetu huyo alikamatwa alhamisi hii mchana. Alikuwa katika eneo la Karuba ndani ya wilaya ya Masisi mkoa wa Kivu-kaskazini mashariki mwa DRC.

” Alikuwa ameniambia kuwa anakwenda kufanya ripoti kuhusu mchakato wa kuwaorodhesha wapiga kura katika eneo la mashariki ambao ungeanza alhamisi hii”, alibaini mwandishi wa habari aliyezungumza na ripota huyo wa VOA kabla ya kwenda uwanjani.

Jimmy Shukrani Bakomera anazuiliwa katika jela moja ya idara ya ujasusi Goma (makao makuu ya Kivu kaskazini).

” ijumaa hii Jimmy atapelekwa mjini Kinshasa. Anatuhumiwa kushirikiana na kundi la M23″, ofisi ya idara ya ujasusi mjini Goma imeliambia gazeti la SOS Médias Burundi.

” Amekatazwa kuzungumza na watu “, ofisi hiyo imezidi kusema.

Januari iliyopita, mwenzetu huyo alijeruhiwa na polisi wakati akiripoti juu ya mandamano dhidi ya kikosi cha EAC mjini Goma. Wandishi wa habari wengine walikamatwa na kujeruhiwa pia. Sauti ya Amerika haijatoa maelezo yoyote kuhusu kukamatwa kwa mwandishi huyo tangu tulipoweka hewani habari hii.

Wandishi wengi wamekamatwa na idara za usalama za Kongo na kuzuiliwa katika gereza la polisi au jeshi pasina kufahamisha waajiri wao au familia.

DRC iko kwenye nafasi ya 125 kwa jumla ya nchi 180 kuhusu kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari katika orodha ya shirika linalotetea haki za wandishi wa habari la maripota wasio na mipaka.

Previous Burundi : authorities arrest the fifth activist, jail the team suspected of funding terrorism
Next Burundi : viongozi wanahakikisha kukamatwa kwa mwanaharakati mwingine na kumuweka gerezani huku timu yote ikituhumiwa kufadhili ugaidi

You might also like

Society

Cibitoke : increase in transport tickets following the hunt for fuel traffickers

Witnesses indicate that transport has become a headache. Basic necessities are on the rise following the measure to suspend illegal fuel trafficking from the DR Congo since Wednesday, July 24.

Human Rights

Prince-Regent Charles : the hard road of the dead to their final rest

For days, Prince Régent Charles Hospital located in the commercial capital Bujumbura has had no place in its morgue for the dead. Families of the deceased are complaining. Sources at

Security

DRC: Maï Maï wanataka kusaidia jeshi la FARDC

Makundi mbali mbali ya Maï Maï yalifahamisha kuwa yanataka kushirikiana na jeshi la Kongo katika vita dhidi ya kundi la M23. Hii ni baada ya rais Tshisekedi siku ya alhamisi