Mahama (Rwanda) : mkimbizi wa Burundi afariki dunia baada ya kupigwa na wakimbizi kutoka Kongo

Mahama (Rwanda) : mkimbizi wa Burundi afariki dunia baada ya kupigwa na wakimbizi kutoka Kongo

Emmanuel Ruremesha aliuwawa jumanne hii tarehe 28 februari. Alifariki kutokana na vipigo alivyofanyiwa wakati wa ugomvi na raia wa Kongo usiku wa kuamkia jumanne hii. Polisi tayari ilikamata watu kadhaa kwa sababu za uchunguzi. HABARI SOS Médias Burundi

Ugomvi iliyosababisha kifo cha Ruremesha ulifanyika katika mgahawa wa pombe ndani ya kambi ya Mahama.

” Alipigwa vibaya hadi damu kutililika mdomoni na puwani” mashahidi walieleza.

Licha ya kupelekwa haraka kwenye hospitali ya ” Save the Children” katika zone ya Mahama ll, alifariki dunia siku moja badaye vyanzo vyetu viliendelea kueleza.

Muili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Kirehe kwa vile wahudumu wa afya ndani ya kambi wakiwa hawana huduma ya kufanya mazishi.

Baada ya tukio hilo, polisi iliingilia kati na kuwasimamisha watu kadhaa kwa lengo la kufanya uchunguzi.

Watu wa karibu na muhanga, wanaomba muhusika wa mauwaji hayo aweze kuadhibiwa kwa mjibu wa sheria.

Tangu tukio hilo, polisi ilizidisha doria katika eneo la tukio. Wanahofu kuwa warundi wanaweza kulipiza kisasi dhidi ya raia wa Kongo.

Amri ya kufunga mapema mgahawa ilitolewa kwa mmiliki wake.

Amekuwa mkimbizi wa Burundi wa nne kuuwawa katika ukanda huo katika mwezi huu. Wakimbizi wengine wa Burundi waliuwawa katika kambi ya Nduta nchini Tanzania na mwingine katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwezi februari ulioyopita.

Previous Rwanda-DRC : jeshi la Rwanda lauwa mwanajeshi wa tatu wa Kongo
Next Mahama (Rwanda) : a Burundian refugee dies after being beaten up by Congolese

You might also like

Security

Uvira: watu sita akiwemo askali jeshi wauwawa katika mapigano kati ya jeshi na kundi la Maï Maï

Wananchi wawili, waasi watatu na askali jeshi mmoja waliuwawa siku ya alhamisi kwenye eneo la Mubere. Ni katika mji wa Kigoma wilaya ya Uvira ndani ya mkoa wa Kivu ya

Refugees

Nduta (Tanzania): a tomb demolished by the administration for the simple reason that it is built of cement

The demolished grave was holding the remainings of a Burundian refugee, buried in the cemetery of zone 9 in Nduta camp. The camp’s top official was supervising. INFO SOS Médias

Refugees

Goma : angalau watoto 16 walifariki dunia kutokana na mazingira mabaya ndani ya kambi mpya ya wakimbizi wa ndani ya Majengo

Watoto wote 16 walifariki dunia katika kipindi cha chini ya wiki mbili. Kituo kinachowapa hifadhi wakimbizi hao wa vita kinapatikana katika kata ya Majengo tarafa ya Karisimbi. Ni katika mji