Gitega : watuhumiwa watano wa mapenzi ya jinsia moja wameachiwa huru kwa jumla ya wale 24 wanaozuiliwa jela
Uamzi wa kuwaachilia huru umechukuwa jumatatu hii tarehe 20 machi, amethibitisha hayo mmoja kati ya mawakili waliotetea kundi hilo. Watano hao walioachiliwa huru walikuwa katika kundi la watu 24 wanaotuhumiwa kufanya mapenzi ya jinsia moja waliosimamishwa mwezi februari uliopita. Wanazuiliwa katika gereza kuu la Gitega (makao makuu ya kisiasa). HABARI SOS Médias Burundi
Ni wanaume wawili na wanawake watatu. Wameachiwa huru kwa muda jumatatu hii , chanzo cha polisi kiliambia SOS Médias Burundi .
” Ni mahakama ya mkoa wa Gitega iliyochukuwa uamzi wa kuwaachilia huru jumatatu hii mchana” , mmoja kati ya mawakili watetezi wa kundi amethibitishia SOS Médias Burundi. Wajumbe wengine wa kundi hilo wamesikilizwa jumanne hii mchana wakiwa katika jela la Gitega. Wanatuhumiwa kosa la kushawishi watu kufanya ulevi”.
Watu wa karibu yao wanaomba waachiliwe huru uchunguzi wa kiafya ukiwa bado kufanyika .
Wote 24 wakiwa ni wapenzi wa jinsia moja walikamatwa tarehe 22 februari wakidiri mafunzo katika mji wa Gitega kabla ya kupelekwa katika jela la mkoa huo tarehe 6 machi iliyopita.