Bujumbura : kazi zavurugika kutokana na umeme unaokatika mara kwa mara
Hali ya umeme kukatika mara kwa mara inaripotiwa katika mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura. Wakaazi wanalalamika huku wafanyabiashara wanaoendesha shughuli za kibiashara wakidai kupata hasara kubwa. Mamlaka ya maji na umeme Regideso bad o haijatoa maelezo. HABARI SOS Medias Burundi
Ni wengi wanaolalamika kutokana na hali hiyo ya umeme kukatika mara kwa mara ndani ya mji wa Bujumbura.
” Tunalazimika kulipa franka elfu moja za ziada kwenye gharama ya kushevu nywele. Ni pesa nyingi wakati uchumi wa nchi ukiwa mbaya “, aliambia SOS Medias Burundi akiwa na hasira mwanamke mmoja aliyekuwa akitoka katika chumba cha kutengeneza nywele za wanawake.
Wanaofanya kazi ya kuchevu nywele wanasema kuwa hali hiyo huwaletea shida na wateja wao sababu hawaelewi tatizo la kutumia mafuta ya gari. Ni bidhaa inayonunuliwa kwa franka nyingi”.
Katika mgahawa wa vyakula pembeni, mrasibu analaani hasara aliyopata katika wiki mbili zilizopita.
” Tunanunua chakula ambacho kitatumiwa kwa siku moja. Ni muda wa asubuhi ambapo tunapata matatizo mengi sababu hatuwezi kuuzisha maziwa. Tulikuwa na uwezo wa kuuzisha hadi lita 15 kwa siku lakini tunalangua tu lita tano ili kujiepusha na hasara ” alihakikisha.
Katika familia ambazo zina mazoea ya kununua vitu vinavyohidhiwa ndani ya frije au jakofu, bidhaa hizo zinaoza siku moja badaye.
Kwa mjibu wa ushuhuda uliotolewa na wandishi wetu, umeme unakatika kwa angalau mara nne kwa siku kabla ya kukatika kwa muda mrefu wakati wa usiku.
” Hatuelewi umuhimu wa Regideso “, wanalaani.
Regideso bado haijajieleza kuhusiana na madai hayo ya wakaazi.
You might also like
Mgogoro wa Mawasiliano nchini Burundi: ABUCO yalaani hatua kutochukuliwa na mamlaka huku huduma zikizorota
SOS Médias Burundi Bujumbura, Julai 31, 2026—Chama cha Watumiaji nchini Burundi (ABUCO) kinatoa tahadhari kuhusu kuzorota kwa huduma za mawasiliano nchini humo. Katika taarifa iliyotolewa Jumanne, Julai 28, 2026, rais
Gitega: athari mbaya za uhaba wa vinywaji vya Brarudi
Msururu mzima wa kazi unaohusiana na vinywaji katika Brasserie et limonaderies du Burundi (Brarudi) umeathiriwa pakubwa na uhaba wa vinywaji hivi. Hii ni kati ya kipakuliwa cha lori hadi kidhibiti
Ujenzi nchini Burundi: mtaalam anaonya juu ya Hatari za kuanguka Kwa sababu ya kutofuata viwango
SOS Médias Burundi Bujumbura, Juni 13, 2026 – Kukosa kufuata viwango vya ujenzi wa majengo, hasa kwa majengo ya orofa nyingi, kunaweza kuhatarisha Burundi katika majanga yanayoweza kuzuilika. Hili ndilo
