Bujumbura : kazi zavurugika kutokana na umeme unaokatika mara kwa mara
Hali ya umeme kukatika mara kwa mara inaripotiwa katika mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura. Wakaazi wanalalamika huku wafanyabiashara wanaoendesha shughuli za kibiashara wakidai kupata hasara kubwa. Mamlaka ya maji na umeme Regideso bad o haijatoa maelezo. HABARI SOS Medias Burundi
Ni wengi wanaolalamika kutokana na hali hiyo ya umeme kukatika mara kwa mara ndani ya mji wa Bujumbura.
” Tunalazimika kulipa franka elfu moja za ziada kwenye gharama ya kushevu nywele. Ni pesa nyingi wakati uchumi wa nchi ukiwa mbaya “, aliambia SOS Medias Burundi akiwa na hasira mwanamke mmoja aliyekuwa akitoka katika chumba cha kutengeneza nywele za wanawake.
Wanaofanya kazi ya kuchevu nywele wanasema kuwa hali hiyo huwaletea shida na wateja wao sababu hawaelewi tatizo la kutumia mafuta ya gari. Ni bidhaa inayonunuliwa kwa franka nyingi”.
Katika mgahawa wa vyakula pembeni, mrasibu analaani hasara aliyopata katika wiki mbili zilizopita.
” Tunanunua chakula ambacho kitatumiwa kwa siku moja. Ni muda wa asubuhi ambapo tunapata matatizo mengi sababu hatuwezi kuuzisha maziwa. Tulikuwa na uwezo wa kuuzisha hadi lita 15 kwa siku lakini tunalangua tu lita tano ili kujiepusha na hasara ” alihakikisha.
Katika familia ambazo zina mazoea ya kununua vitu vinavyohidhiwa ndani ya frije au jakofu, bidhaa hizo zinaoza siku moja badaye.
Kwa mjibu wa ushuhuda uliotolewa na wandishi wetu, umeme unakatika kwa angalau mara nne kwa siku kabla ya kukatika kwa muda mrefu wakati wa usiku.
” Hatuelewi umuhimu wa Regideso “, wanalaani.
Regideso bado haijajieleza kuhusiana na madai hayo ya wakaazi.
You might also like
Burundi: bei ya sukari isiyoweza kupatikana iliongezeka kwa karibu mara tatu
Bei ya kilo moja ya sukari kwa muuzaji reja reja inapanda hadi faranga za Burundi 8,000 huku ilinunuliwa kwa 3,500 kampuni ya serikali pekee inayohusika na uzalishaji wa sukari, inasema
Kayanza: kukatika kwa umeme kunapooza jiji, tafakari ya shida ya kitaifa ya nishati
Huko Kayanza kaskazini mwa Burundi, kama ilivyo katika maeneo mengi ya nchi, kukatika kwa umeme kunazidi kuwa jambo la kawaida. Kwa wiki kadhaa, jiji limekuwa katika mwendo wa polepole. Shughuli
Rumonge: mgogoro wa kisheria kati ya wapangaji na wamiliki wa vibanda katika soko kuu la mkoa
Wakati masoko ya kisasa yameanguka chini ya uendeshaji wa OBR (Ofisi ya Mapato ya Burundi), mzozo wa kisheria umeibuka katika kesi ya soko kuu la Rumonge (kusini-magharibi mwa Burundi). Na
