Rutana: mfuasi mwenye ushawishi wa chama cha CNDD-FDD akungwa mwaka mmoja jela
Nestor Butisi Nibigira mfanyabiashara na mfuasi mwenye ushawishi wa chama cha CNDD-FDD tarafani Giharo amekatiwa kifungo cha mwaka mmoja jela. Atalazimika kulipa faini ya milioni 2.5 sarafu za burundi. Uamzi umechukuliwa jumatano hii alasiri baada ya kesi dhidi yake asubuhi ya hiyo siku katika korti ya Rutana (Kusini mashariki mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi
Mtuhumiwa aliripoti mbele ya jopo la majaji wa korti ya mkoa wa Rutana jumatatu ambalo limeamuru asalie gerezani.
” Kesi dhidi yake, iliharakishwa zaidi ya kesi za wafungwa wengine”, chanzo kwenye korti ya Rutana kinahakikisha.
Katika siku mbili peke, aliripoti mbele ya jopo la majaji na kesi yake kusikilizwa. Maanuzi yalichukuliwa siku hiyo hiyo.
“Vigogo wa chama cha CNDD-FDD waliwashawishi majaji , waliwapa maelekezo ” , chanzo karibu na faili hiyo kinaeleza.
Nestor Butisi Nibigira alikuwa alisimamishwa na polisi baada ya msako wa tarehe 24 oktoba. Mifuko 35 ya mbolea ya kizungu, 17 ya sukari na jerikani 9 za pombe haramu vilikamatwa kwenye duka lake na nyumbani kwake.
Mfuasi huyo na mwenye ushawishi wa chama tawala anafahamika katika tarafa ya Giharo kama mtu aliyeshiriki katika kamata kamata ya kiholela ya wa upinzani hasa wafuasi wa chama cha CNL.
Kosa peke la ubadilifu na biashara haramu ndilo lilizingatiwa dhidi yake.
You might also like
DRC (North Kivu): the M23 returns to old positions
The March 23 Movement (M23) has recaptured localities that it had ceded as part of the ceasefire demanded by the Heads of State of the East African Community since December
Burunga : journalists excluded and suspicions of orchestrated restrictions at a ruling party meeting
SOS Médias Burundi Burunga, May 12, 2026—Tensions persist regarding journalists’ access to public and political activities in Burunga province. Several reporters are denouncing repeated exclusions and restrictions on media coverage
Crise dans l’Est du Congo : un casque bleu tué et un autre gravement blessé dans une attaque contre un avion de la Monusco
La Monusco (Mission de l’organisation des Nations-Unies en RDC) a annoncé la mort de son casque bleu dans un communiqué. Elle informe qu’il est décédé à la suite de l’attaque
