Kirundo: Imbonerakure auwawa na wenzake

Kirundo: Imbonerakure auwawa na wenzake

Mwanaume wa miaka 41 aliuwawa asubuhi ya siku ya alhamisi eneo la Rwimbogo kijiji cha Rushubuje tarafa ya Ntega (Mkoa wa Kirundo kaskazini mwa Burundi). Muhanga huyo aliyekuwa Imbonerakure (Kijana mjumbe wa tawi la vijana wa chama tawala cha CNDD-FDD) alipigwa vikali na wenzake kwa tuhma za kuvunja Siri kuhusu makosa yanayofanywa na kundi. HABARI SOS Médias Burundi

Habiyambere (miaka 41) alikamatwa na kundi la Imbonerakure usiku wa jumatano majira ya saa nne za usiku.

Vijana hao Imbonerakure ambao kiongozi wao ni Nzobarinda alikuwa akiwashambulia mwanaume na mwaname mmoja waliokuwa wakiongea baada ya kwenda kwenye kilabu cha pombe.

“Habiyambere alikuwa amekuja kumtafuta mkubwa wa Imbonerakure katika eneo la Rwimbogo kwa jina la Nzobarinda ambaye walikuwa wakiendesha wizi kwa pamoja”, vyanzo vya ndani vinasema.

Alimuuliza wapi alikuwa anakwenda nyakati hizo za saa nne na akajibu kuwa anakwenda kwake Nzobarinda.

Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, Nzobarinda alikuwa na chuki dhidi yake sababu alikuwa akituhumu kuvunja siri, yeye na Imbonerakure wengine wanafanya wizi usiku wakiwa na mkuu wa Imbonerakure.

Nzobarinda aliamuru Imbonerakure wengine kumpa ” adhabu”

” Hata atakata pumzi yake ya mwisho. Nitajihusisha na ya kufuatia” alihakikisha Nzobarinda.

walimpiga muhanga na kumuacha eneo hilo akiwa mahtuti.
” Hatuelewi namna aliweza kufika kwake. Majira ya saa nane za usiku alhamisi, tulimupeleka kwenye kituo cha afya akiwa katika hali mbaya. Alikuwa akitapika na kukojoa damu. Alifariki majira ya saa kumi na moja za asubuhi kwenye kituo hicho cha afya” alithibitisha mjumbe wa familia yake.

Familia ya muhanga inaomba sheria ifanye kazi.

” Waliohusika wanajulikana. Hadi sasa vyombo vya sheria bado kuwajibika na kuwakamata watuhumiwa.

Watuhumiwa wanasema kuwa muhanga alifumaniwa akijaribu kutoboa nyuma ili aweze kuingia na kuiba ndani.

Shirika la ndani la haki za binadamu linaomba waliofanya mauwaji hayo wakamatwe mara moja. Yanaomba pia kiongozi wa tarafa ya Ntega , Pierre Claver Mbanzabugabo kuacha ukimya wake sababu tarafa hiyo imekuwa uwanja wa mauwaji.

Viongozi wa tarafa hawajasema lolote kuhusiana na madai hayo.

Previous Kirundo: an Imbonerakure killed by his peers
Next Nduta: watu 10 wanaomba hifadhi wazuiliwa jela

You might also like

Security

Masisi : hofu imetanda eneo la Sake kutokana na mapigano kati ya jeshi na kundi la M23

Hali ya taharuki imeshuhudiwa alhamisi hii ndani ya jiji la Sake kwenye umbali wa takriban kilometa 20 magharibi ya mji wa Goma( makao makuu ya mkoa wa Kivu kaskazini) mashariki

Security

Nairobi: the protagonists in the Congolese crisis meet without the M23

Since Monday, November 28, a meeting is talking place in Nairobi, for six days without the M23, to deal with the Congolese crisis. The M23, a rebel movement which seized

Security

Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC

Wanajeshi hao watatu waliuwawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na kundi la silaha la Twirwaneho linaloundwa na vijana wa jamii ya Banyamulenge, jumanne hii. HABARI SOS Médias Burundi