Kirundo: Imbonerakure auwawa na wenzake

Kirundo: Imbonerakure auwawa na wenzake

Mwanaume wa miaka 41 aliuwawa asubuhi ya siku ya alhamisi eneo la Rwimbogo kijiji cha Rushubuje tarafa ya Ntega (Mkoa wa Kirundo kaskazini mwa Burundi). Muhanga huyo aliyekuwa Imbonerakure (Kijana mjumbe wa tawi la vijana wa chama tawala cha CNDD-FDD) alipigwa vikali na wenzake kwa tuhma za kuvunja Siri kuhusu makosa yanayofanywa na kundi. HABARI SOS Médias Burundi

Habiyambere (miaka 41) alikamatwa na kundi la Imbonerakure usiku wa jumatano majira ya saa nne za usiku.

Vijana hao Imbonerakure ambao kiongozi wao ni Nzobarinda alikuwa akiwashambulia mwanaume na mwaname mmoja waliokuwa wakiongea baada ya kwenda kwenye kilabu cha pombe.

“Habiyambere alikuwa amekuja kumtafuta mkubwa wa Imbonerakure katika eneo la Rwimbogo kwa jina la Nzobarinda ambaye walikuwa wakiendesha wizi kwa pamoja”, vyanzo vya ndani vinasema.

Alimuuliza wapi alikuwa anakwenda nyakati hizo za saa nne na akajibu kuwa anakwenda kwake Nzobarinda.

Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, Nzobarinda alikuwa na chuki dhidi yake sababu alikuwa akituhumu kuvunja siri, yeye na Imbonerakure wengine wanafanya wizi usiku wakiwa na mkuu wa Imbonerakure.

Nzobarinda aliamuru Imbonerakure wengine kumpa ” adhabu”

” Hata atakata pumzi yake ya mwisho. Nitajihusisha na ya kufuatia” alihakikisha Nzobarinda.

walimpiga muhanga na kumuacha eneo hilo akiwa mahtuti.
” Hatuelewi namna aliweza kufika kwake. Majira ya saa nane za usiku alhamisi, tulimupeleka kwenye kituo cha afya akiwa katika hali mbaya. Alikuwa akitapika na kukojoa damu. Alifariki majira ya saa kumi na moja za asubuhi kwenye kituo hicho cha afya” alithibitisha mjumbe wa familia yake.

Familia ya muhanga inaomba sheria ifanye kazi.

” Waliohusika wanajulikana. Hadi sasa vyombo vya sheria bado kuwajibika na kuwakamata watuhumiwa.

Watuhumiwa wanasema kuwa muhanga alifumaniwa akijaribu kutoboa nyuma ili aweze kuingia na kuiba ndani.

Shirika la ndani la haki za binadamu linaomba waliofanya mauwaji hayo wakamatwe mara moja. Yanaomba pia kiongozi wa tarafa ya Ntega , Pierre Claver Mbanzabugabo kuacha ukimya wake sababu tarafa hiyo imekuwa uwanja wa mauwaji.

Viongozi wa tarafa hawajasema lolote kuhusiana na madai hayo.

Previous Kirundo: an Imbonerakure killed by his peers
Next Nduta: watu 10 wanaomba hifadhi wazuiliwa jela

You might also like

Security

Goma: large-scale protests

The city of Goma (capital of North Kivu, eastern DRC) woke up in great tension on Monday morning following a protest against the regional force of the EAC. The protesters

Security

Gitega : a person kidnapped and tortured by a local administration officer in complicity with Imbonerakure

Asman Rwasa, 32 years old, was kidnapped and then tortured by the Yoba neighborhood chief in Gitega, the political capital of Burundi, with the complicity of certain Imbonerakure (members of

Security

Ituri: watu takriban 30 wameuwawa eneo la Djugu

Shumbulio jingine la mauwaji lilifanywa na kundi la CODECO ( shirikisho kwa ajili ya maendeleo ya Kongo) katika wilaya ya Djugu Kijiji cha Bahema-Banywagi kwenye kitongoji cha Nyamamba wekendi hii.