Mkutano wa Nairobi: wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge waajiondoa katika mazungumzo
Wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge walisusia mazungumzo ya Nairobi tangu alhamisi. Hoja, ni shambulio lililosababisha vifo vya watu saba wajumbe wa jamii hiyo mkoa wa kivu-kusini (Mashariki mwa RDC) tarehe 30 novemba. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na tangazo la siku ya alhamisi, wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge wanasema ni hali ambayo hawawezi kuvumilia na kukubali.
Wanalaani shambulio hilo la kundi la Mai Mai kwa ushirikiano na waasi kutoka Burundi wa Red Tabara katika milima mirefu ya Minembwe mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa DRC.
” Watu saba waliuwawa katika shambulio hilo na 10 wengine kujeruhiwa” kulingana na tangazo la wawakilishi wa jamii hiyo.
Wanaomba serikali ya Kongo na mpatanishi wa EAC ” kulaani shambulio hilo la 30 novemba na mashambulizi mengine yanayofanyika katika wilaya ya Mwenga, Uvira, Itongwe na Fizi tangu april 2017 na ambayo malengo yake ni kutokomeza kabila “
Mazungumzo hayo hata hivyo yalicheleweshwa kwa masaa mengi siku ya alhamisi. Ujumbe kutoka serikali ya Kongo walipata wasi wasi kuwa siri za mjadala wawo zinavuja kuelekea nchi jirani kupitia vifaa vilivyowekwa ndani ya mitambo ya kutafsiri lugha, walihakikishia SOS Media Burundi washiriki katika vikao hivyo.
” Tunaomba yafukuzwe makundi ya silaha yaliyosababisha mauwaji hayo na adhabu zichukuliwe dhidi yao sawa na yale yaliokubaliwa na pande zote zinazoshiriki mazungumzo hayo na kutanzagwa rasmi na mjumbe maluum wa rais katika mazungumzo hayo” alifafanua Enock Ruberangabo, mmoja wa wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge mjini Nairobi.
Kwa mjibu wake, “Haina maana yoyote kuendelea na mazungumzo wakati mashambulizi yakiendelea uwanjani, kinyume na walichoafikiana.”
You might also like
Eastern DRC : intensification of military operations and rising tensions in the highlands
SOS Médias Burundi Uvira, May 19, 2026 – The security situation continues to deteriorate in the highlands of South Kivu, in the Democratic Republic of Congo, amid intensified military operations
DRC : Corneille Nangaa and his entourage sanctioned by the United States
In a statement released on Thursday, the United States of America announced that it had taken sanctions against Corneille Nangaa, head of the Congo River Alliance (AFC) and some of
Rumonge : a body floating on Lake Tanganyika discovered
The body of Emmanuel Nduwimana (46 years old) was found very close to the commercial port of Rumonge on Tuesday, June 25, 2024. His corpse was floating on the waters
