Mkutano wa Nairobi: wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge waajiondoa katika mazungumzo
Wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge walisusia mazungumzo ya Nairobi tangu alhamisi. Hoja, ni shambulio lililosababisha vifo vya watu saba wajumbe wa jamii hiyo mkoa wa kivu-kusini (Mashariki mwa RDC) tarehe 30 novemba. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na tangazo la siku ya alhamisi, wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge wanasema ni hali ambayo hawawezi kuvumilia na kukubali.
Wanalaani shambulio hilo la kundi la Mai Mai kwa ushirikiano na waasi kutoka Burundi wa Red Tabara katika milima mirefu ya Minembwe mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa DRC.
” Watu saba waliuwawa katika shambulio hilo na 10 wengine kujeruhiwa” kulingana na tangazo la wawakilishi wa jamii hiyo.
Wanaomba serikali ya Kongo na mpatanishi wa EAC ” kulaani shambulio hilo la 30 novemba na mashambulizi mengine yanayofanyika katika wilaya ya Mwenga, Uvira, Itongwe na Fizi tangu april 2017 na ambayo malengo yake ni kutokomeza kabila “
Mazungumzo hayo hata hivyo yalicheleweshwa kwa masaa mengi siku ya alhamisi. Ujumbe kutoka serikali ya Kongo walipata wasi wasi kuwa siri za mjadala wawo zinavuja kuelekea nchi jirani kupitia vifaa vilivyowekwa ndani ya mitambo ya kutafsiri lugha, walihakikishia SOS Media Burundi washiriki katika vikao hivyo.
” Tunaomba yafukuzwe makundi ya silaha yaliyosababisha mauwaji hayo na adhabu zichukuliwe dhidi yao sawa na yale yaliokubaliwa na pande zote zinazoshiriki mazungumzo hayo na kutanzagwa rasmi na mjumbe maluum wa rais katika mazungumzo hayo” alifafanua Enock Ruberangabo, mmoja wa wawakilishi wa jamii ya Banyamulenge mjini Nairobi.
Kwa mjibu wake, “Haina maana yoyote kuendelea na mazungumzo wakati mashambulizi yakiendelea uwanjani, kinyume na walichoafikiana.”
You might also like
Minembwe: mwanajeshi amuuwa mwanafunzi kwa panga
Mugaza Nganganyi (Miaka 16) aliuwawa jumapili hii. Ni mwanajeshi wa FARDC (Jeshi la jamuhuri ya Kongo) aliyemuuwa kulingana na familia yake. Alimufananisha na raia wa Rwanda. Muhanga ni mjumbe wa
DRC war: Uganda to deploy troops to Goma
The news was announced by the Ugandan army spokesperson on his Twitter account this Thursday, November 17. He says that troops from his country will arrive in the near future
Beni : the civil society warns of the slackening of joint FARDC-UPDF operations
The bureau of the civil society Forces Vives of the Rwenzori sector in Beni territory in North Kivu in eastern DRC warns of the slackening of joint operations by the
