Beni: waasi nane wa ADF wauwawa
Jeshi la Kongo linafahamisha kuwa liliwauwa waasi nane na kuwakamata wengine 5 wa ADF (kundi la waasi wa Uganda) alhamisi hii katika kijiji cha Kisasu Ngandu. Ni katika wilaya ya Beni mkoa wa Kivu-kaskazini (mashariki mwa DRC). HABARI SOS Médias Burundi
Ni msemaji wa kikosi cha Sokola 1, kaskazini-kubwa aliyefahamisha hayo.
” Ni matokeo ya mapigano kati ya watu wetu na kundi la ADF katika usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa kusini mwa eneo la Karuruma katika kijiji cha Bashi. Kwenye eneo la mapigano magaidi watatu wa ADF waliuwawa moja kwa moja. Miili mingine mitano ilipatikana baada ya mapigano”, aliripoti kepteni Antony Mualushayi.
Anazidi kuwa silaha aina ya AK-47 na vifaa vya mawasiliano vilikamatwa pia.
[…], baada ya kushindwa, aduwi alielekea katika mbuga ya wanyama ya Virunga. Tunawaomba raia wakaazi wa karibu na hifadhi hiyo ya kimataifa kuwa makini”, alizidi kusema.
” Kikundi cha ADF kwa sasa linakabiliwa na mashambulizi ya jeshi huku kikijaribu kulipiza kisasi wakati huu wa siku kuu. Huduma zetu maalum zilifichua mtandao wa magaidi wa ADF uliokuwa ikiandaa mashambulizi dhidi ya mji wa Béni “, alimalizia.
You might also like
DRC : the standoff between President Tshisekedi and the M23 is not ready to end
On Wednesday September 20, 2023, the Congolese president declared to the press in New York that he does not intend to dialogue with the M23 rebels. The latter seems to
Cibitoke: Rwandan FLN rebels sow fear among the population near Kibira
For two weeks now, residents of the hills near Kibira, Gafumbegeti and Rutorero Butahana zone of Mabayi commune, Cibitoke province, have said they are in panic fear of the Rwandan
Gihanga : three police officers arrested in possession of fraudulent goods
Three police officers in a vehicle were arrested and goods in their possession seized by their colleagues. They only stopped the car after warning shots were fired this Sunday evening
