Beni: waasi nane wa ADF wauwawa

Beni: waasi nane wa ADF wauwawa

Jeshi la Kongo linafahamisha kuwa liliwauwa waasi nane na kuwakamata wengine 5 wa ADF (kundi la waasi wa Uganda) alhamisi hii katika kijiji cha Kisasu Ngandu. Ni katika wilaya ya Beni mkoa wa Kivu-kaskazini (mashariki mwa DRC). HABARI SOS Médias Burundi

Ni msemaji wa kikosi cha Sokola 1, kaskazini-kubwa aliyefahamisha hayo.

” Ni matokeo ya mapigano kati ya watu wetu na kundi la ADF katika usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa kusini mwa eneo la Karuruma katika kijiji cha Bashi. Kwenye eneo la mapigano magaidi watatu wa ADF waliuwawa moja kwa moja. Miili mingine mitano ilipatikana baada ya mapigano”, aliripoti kepteni Antony Mualushayi.

Anazidi kuwa silaha aina ya AK-47 na vifaa vya mawasiliano vilikamatwa pia.

[…], baada ya kushindwa, aduwi alielekea katika mbuga ya wanyama ya Virunga. Tunawaomba raia wakaazi wa karibu na hifadhi hiyo ya kimataifa kuwa makini”, alizidi kusema.

” Kikundi cha ADF kwa sasa linakabiliwa na mashambulizi ya jeshi huku kikijaribu kulipiza kisasi wakati huu wa siku kuu. Huduma zetu maalum zilifichua mtandao wa magaidi wa ADF uliokuwa ikiandaa mashambulizi dhidi ya mji wa Béni “, alimalizia.

Previous Cibitoke: kilio cha raia waliofanyiwa mateso na kusikilizwa katika gereza la SNR mkoani
Next Minembwe: jeshi la Kongo na kundi la Twirwaneho walipoteza watu 11

You might also like

Security

North Kivu: renewal of fighting between the FARDC and the M23 in Rutshuru

New clashes between the Armed Forces of the Democratic Republic of Congo (FARDC) and the M23 have broke out since Friday morning in several villages in the territory of Rutshuru,

Human Rights

Nyarugusu (Tanzania): several maize fields destroyed by the camp administration

The incidents occurred since early this week at the Nyarugusu camp in Tanzania. The refugee camp managers destroyed maize fields to discourage farming activity.The refugees speak of “a crime assumed”.

Security

Nyarugusu (Tanzania): mkimbizi mwenye asili ya Burundi alipatikana akiwa maiti

Mkimbizi kutoka Burundi mwenye umri wa miaka takriban miaka 40 aliuwawa na watu wasiojulikana karibu ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu nchini Tanzania. Polisi inasema ni tukio la wizi lililokwenda