Beni: waasi nane wa ADF wauwawa
Jeshi la Kongo linafahamisha kuwa liliwauwa waasi nane na kuwakamata wengine 5 wa ADF (kundi la waasi wa Uganda) alhamisi hii katika kijiji cha Kisasu Ngandu. Ni katika wilaya ya Beni mkoa wa Kivu-kaskazini (mashariki mwa DRC). HABARI SOS Médias Burundi
Ni msemaji wa kikosi cha Sokola 1, kaskazini-kubwa aliyefahamisha hayo.
” Ni matokeo ya mapigano kati ya watu wetu na kundi la ADF katika usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa kusini mwa eneo la Karuruma katika kijiji cha Bashi. Kwenye eneo la mapigano magaidi watatu wa ADF waliuwawa moja kwa moja. Miili mingine mitano ilipatikana baada ya mapigano”, aliripoti kepteni Antony Mualushayi.
Anazidi kuwa silaha aina ya AK-47 na vifaa vya mawasiliano vilikamatwa pia.
[…], baada ya kushindwa, aduwi alielekea katika mbuga ya wanyama ya Virunga. Tunawaomba raia wakaazi wa karibu na hifadhi hiyo ya kimataifa kuwa makini”, alizidi kusema.
” Kikundi cha ADF kwa sasa linakabiliwa na mashambulizi ya jeshi huku kikijaribu kulipiza kisasi wakati huu wa siku kuu. Huduma zetu maalum zilifichua mtandao wa magaidi wa ADF uliokuwa ikiandaa mashambulizi dhidi ya mji wa Béni “, alimalizia.
You might also like
Ituri : nearly 30 ADF attackers killed, others captured and hostages released, according to the army
The Congolese army has taken stock of its operations during the month of January 2023 in Ituri province (eastern DRC). It claims to have killed 28 and captured 14 ADF
Bujumbura: a policeman shot a man
Olivier Nkeramihigo was shot by a police officer during the night from Friday to Saturday. The incident took place in a bar located in the Ngagara zone in the district
Bujumbura rocked by explosions in Musaga : projectiles hit homes, the population on alert
SOS Médias Burundi Bujumbura, March 31, 2026 — Explosions were heard Tuesday evening in southern Bujumbura, mainly in the Musaga zone, causing many families to flee and panic in several
