Gahuna: jeshi la FARDC na FDND wamesimamisha watu watano wakiwemo warundi wawili
Watu hao watano raia wa kawaida walisimamishwa jumamosi hii majira ya alasiri : wanatuhumiwa kumuhudumia kanali Makanika, kamanda wa kundi la Twirwaneho linaloundwa na watu wa jamii ya Banyamulenge. HABARI SOS Médias Burundi
Watu hao walikuwa wakielekea katika eneo la Nyawaranga. Ni katika kijiji cha Bijombo, wilaya ya Uvira ( mkoa wa kivu ya kusini mashariki mwa DRC), kwa mjibu wa vyanzo vya ndani.
Visa hivyo vilitokea katika kijiji cha Kibogero.
” Ni wachungaji wawili, raia wa Kongo kutoka jamii ya Bashi, mkuu wa kijiji cha Gahuna pamoja na kijana ambaye ni kati ya walinzi wa karibu wa kanali Makanika” , vyanzo vya kijeshi vinasema.
Kulingana na vyanzo eneo la Bijombo, wapiganaji wa Twigwaneho walitoa amri kwa watu hao waliokuwa wanazuiliwa ” kubeba vyakula hadi eneo la Nyawaranga”.
Taarifa kutoka katika vyanzo vya jeshi zinahakikisha kuwa wahusika wanazuiliwa katika mji wa Uvira.
Kulingana na wandishi wetu, katika eneo hilo la Kongo ambako makundi ya silaha ya ndani na nje kutoka Burundi yalipiga kambi, makundi ya waasi yanatumia raia wa kawaida kubeba vyakula na risasi, eneo hilo likiwa halina barabara.
FDNB ( jeshi la Burundi) liko katika ardhi ya Kongo rasmi tangu agosti 2022. Wanapatika eneo hilo chini ya mwamvuli wa kikosi cha kikanda cha EAC kilichoanzishwa na wakuu wa nchi za jumuiya ya afrika mashariki juni mwaka jana. Lakini jeshi la Burundi kwa miaka mingi linatuhumiwa kuingia kwenye ardhi ya Kongo wakiwa pamoja na vijana wafuasi wa tawi la vijana la chama tawala cha CNDD-FDD kulenga hususan kundi la FNL( waasi wa Burundi) na Red-Tabara, kundi linalochukuliwa na viongozi wa Burundi kama kundi la kigaidi, makundi hayo mawili yakiwa yalipiga kambi eneo la Kivu kusini.
Katika miezi iliyopita, mapigano kati ya jeshi la Burundi na makundi hayo mawili ya silaha yaliripotiwa eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini na kila upande ukidai kupata ushindi.
You might also like
Buganda: kijana Imbonerakure auwawa na mwanajeshi
Kisa hicho kilitokea alhamisi hii kwenye transversale ya nne katika kijiji cha Nyamitanga mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Mwanajeshi alimpiga risasi kijana Imbonerakure (mfuasi wa tawi la vijana la
Gahuna: FARDC and FDNB arrested five people including two Burundians
The five individuals were arrested this Saturday at the beginning of the afternoon. They are suspected of supplying fallen Colonel Makanika, commander of the Twirwaneho armed group made up of
Ituri : nearly 30 ADF attackers killed, others captured and hostages released, according to the army
The Congolese army has taken stock of its operations during the month of January 2023 in Ituri province (eastern DRC). It claims to have killed 28 and captured 14 ADF
