Buganda: kijana Imbonerakure auwawa na mwanajeshi
Kisa hicho kilitokea alhamisi hii kwenye transversale ya nne katika kijiji cha Nyamitanga mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Mwanajeshi alimpiga risasi kijana Imbonerakure (mfuasi wa tawi la vijana la chama cha CNDD-FDD). Alifariki papo hapo. Muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muathiriwa ni kijana mwanafunzi aliyekuwa akielekea kumalika masomo mwaka ujao. Kwa mjibu wa mashahidi, ilikuwa majira ya saa moja ambapo Lahay Roy Niyera aliuwawa.
” Alikuwa akijaribu kuondoa udongo katika barabara ili kuruhusu nenda rudi ya magari. Alichafua bila kutaka mwanajeshi na akamuwashia moto. Alifariki katika eneo la tukio”, mashahidi walibaini.
Wanafahamisha kuwa waakazi wengi wakiwemo vijana wa CNDD-FDD waliingilia kati na kutaka kujichukulia sheria mikononi lakini mwanajeshi mwingine akaingilia kati.
Afisa katika FDNB ( jeshi la ulinzi wa taifa la Burundi) anayehusika na operesheni katika eneo hilo, alifahamisha kuwa muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa.
” atahukumiwa kwa mjibu wa sheria”.
Kisa hicho kiliibua mvutano mkali kati ya mwanajeshi na wakaazi wa Nyamitanga. Nenda rudi ilisimama kwa muda wa masaa matano. Hali hiyo ilimalizika baada viongozi tawala na maafisa wa jeshi kuingilia kati.
Wakaazi wanaomba mwanajeshi huyo aliyehusika na kifo hicho ahukumiwe katika kesi ya mafumanio
You might also like
Gatumba attack : the government reveals an alarming death toll
This Saturday afternoon, Jérôme Niyonzima, spokesperson for the Burundian government, announced the sad news of the loss of 20 lives in Vugizo, in the Gatumba zone in western Burundi, not
Kivu-kaskazini: Jeshi na kundi la M23 wanapigana eneo la Rutshuru karibu na RN2
Mapigano kati ya jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo na kundi la machi 23 yameshika kasi alhamisi hii 27 oktoba 2022 katika maeneo ya Chimirwa kwa takriban kilometa 4
Gihanga : a soldier killed a young man and injured a sixty-year-old
The murder took place in the Gihungwe region in Gihanga district of Bubanza province (west). A soldier shot two people. Witnesses speak of an argument between a soldier and two
