Buganda: kijana Imbonerakure auwawa na mwanajeshi
Kisa hicho kilitokea alhamisi hii kwenye transversale ya nne katika kijiji cha Nyamitanga mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Mwanajeshi alimpiga risasi kijana Imbonerakure (mfuasi wa tawi la vijana la chama cha CNDD-FDD). Alifariki papo hapo. Muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muathiriwa ni kijana mwanafunzi aliyekuwa akielekea kumalika masomo mwaka ujao. Kwa mjibu wa mashahidi, ilikuwa majira ya saa moja ambapo Lahay Roy Niyera aliuwawa.
” Alikuwa akijaribu kuondoa udongo katika barabara ili kuruhusu nenda rudi ya magari. Alichafua bila kutaka mwanajeshi na akamuwashia moto. Alifariki katika eneo la tukio”, mashahidi walibaini.
Wanafahamisha kuwa waakazi wengi wakiwemo vijana wa CNDD-FDD waliingilia kati na kutaka kujichukulia sheria mikononi lakini mwanajeshi mwingine akaingilia kati.
Afisa katika FDNB ( jeshi la ulinzi wa taifa la Burundi) anayehusika na operesheni katika eneo hilo, alifahamisha kuwa muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa.
” atahukumiwa kwa mjibu wa sheria”.
Kisa hicho kiliibua mvutano mkali kati ya mwanajeshi na wakaazi wa Nyamitanga. Nenda rudi ilisimama kwa muda wa masaa matano. Hali hiyo ilimalizika baada viongozi tawala na maafisa wa jeshi kuingilia kati.
Wakaazi wanaomba mwanajeshi huyo aliyehusika na kifo hicho ahukumiwe katika kesi ya mafumanio
You might also like
Goma : agglomerations of Kishali and Ihula fall into the hands of M23
Since Wednesday, October 23, the M23 has controlled agglomerations of Kishali and Ihula in Walikale territory. It was after violent fighting that opposed the armed group and the FARDC and
Gitega : two people killed
Désiré Kwizerimana (40 years old), died from injuries inflicted on him by two soldiers, on January 16 at the hospital in Gitega (political capital). A second individual died while he
Bujumbura: a woman’s corpse discovered
A body of a woman was discovered on Monday in the Ngagara zone north of the commercial city Bujumbura. It was taken to the mortuary of Roi Khaled Hospital. INFO
