Buganda: kijana Imbonerakure auwawa na mwanajeshi
Kisa hicho kilitokea alhamisi hii kwenye transversale ya nne katika kijiji cha Nyamitanga mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Mwanajeshi alimpiga risasi kijana Imbonerakure (mfuasi wa tawi la vijana la chama cha CNDD-FDD). Alifariki papo hapo. Muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muathiriwa ni kijana mwanafunzi aliyekuwa akielekea kumalika masomo mwaka ujao. Kwa mjibu wa mashahidi, ilikuwa majira ya saa moja ambapo Lahay Roy Niyera aliuwawa.
” Alikuwa akijaribu kuondoa udongo katika barabara ili kuruhusu nenda rudi ya magari. Alichafua bila kutaka mwanajeshi na akamuwashia moto. Alifariki katika eneo la tukio”, mashahidi walibaini.
Wanafahamisha kuwa waakazi wengi wakiwemo vijana wa CNDD-FDD waliingilia kati na kutaka kujichukulia sheria mikononi lakini mwanajeshi mwingine akaingilia kati.
Afisa katika FDNB ( jeshi la ulinzi wa taifa la Burundi) anayehusika na operesheni katika eneo hilo, alifahamisha kuwa muhusika wa mauwaji hayo alikamatwa.
” atahukumiwa kwa mjibu wa sheria”.
Kisa hicho kiliibua mvutano mkali kati ya mwanajeshi na wakaazi wa Nyamitanga. Nenda rudi ilisimama kwa muda wa masaa matano. Hali hiyo ilimalizika baada viongozi tawala na maafisa wa jeshi kuingilia kati.
Wakaazi wanaomba mwanajeshi huyo aliyehusika na kifo hicho ahukumiwe katika kesi ya mafumanio
You might also like
Kayanza : a man attacks and injures his parents with a machete
A 32-year-old man brutally attacked his parents. He wounded his father and mother with a machete. The incident took place on the night of March 5 to 6 in the
Kirundo: Imbonerakure auwawa na wenzake
Mwanaume wa miaka 41 aliuwawa asubuhi ya siku ya alhamisi eneo la Rwimbogo kijiji cha Rushubuje tarafa ya Ntega (Mkoa wa Kirundo kaskazini mwa Burundi). Muhanga huyo aliyekuwa Imbonerakure (Kijana
Mabayi : a large quantity of food intended to supply Rwandan rebels intercepted
Soldiers on patrol in the Kibira natural reserve in Gafumbegeti village, in the Butahana zone of Mabayi district, Cibitoke province (northwest Burundi) arrested five people in possession of more than
