Cibitoke: watu 15 walipatikana na ugongwa wa kipindipindu kwa kipindi cha chini ya wiki mbili eneo la Rugombo

Cibitoke: watu 15 walipatikana na ugongwa wa kipindipindu kwa kipindi cha chini ya wiki mbili eneo la Rugombo

Janga la kipindipindu linaripotiwa katika eneo la Mparambo tarafani Rugombo mkoa wa Cibitoke (kaskazini magharibi mwa Burundi) tangu wiki mbili zilizopita. Wagonjwa 15 walipatikana. Ukosefu wa maja safi ndio chanzo cha ugonjwa huo. Maafisa wa afya katika mkoa wa Cibitoke wanafahamisha kuwa hawajuwi ulikotoka ugonjwa huo. HABARI SOS Médias Burundi

Visa vya maradhi ya kipindipindu vinaripotiwa mnamo siku chache zilizopita katika eneo la mkoa wa Cibitoke kwenye mwambao wa mto wa Rusizi, unatofautisha nchi za Burundi na DRC. Angalau watu 15 waliopatikana na ugonjwa huo walipokelewa katika huduma ya dharura ya kituo cha afya cha Rugombo.

Wagonjwa wote kulingana na vyanzo katika utawala wanatoka katika kijiji cha Mparambo I tarafani Rugombo kwenye umbali wa kilometa kumi kutoka makao makuu ya mkoa.

Shirika la waganga wa msalaba mwekundu ambalo linatoa huduma zote lilikabidhi pia kituo hicho cha afya gari la wagonjwa kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa wagonjwa.

Shirika la msalaba mwekundu la Burundi na kikosi cha polisi cha kukinga majanga wanawajibika kwa kasi kunyunyizia dawa ndani ya majumba ambako wagonjwa wanaishi. Nyumba zote katika eneo hilo zimepewa huduma ya maji safi.

Regideso ( mamlaka ya umaa ya maji na umeme) inashiriki pia ili maji safi yapatikane. Eneo lililoathiriwa linakabiliwa na ukosefu wa huduma hiyo.

Viongozi wa afya mkoani Cibitoke wanafahamisha kuwa kampeni ya kuwahamasisha raia imeanza kwa ushirikiano na viongozi tawala.

” ni kutokana na uhaba wa maji safi ambapo ugonjwa huo uliripuka”, wanasema.

Previous Cibitoke: 15 people affected with cholera in less than two weeks in Rugombo
Next Buganda: kijana Imbonerakure auwawa na mwanajeshi

You might also like

Health

Burundi : in very critical condition, the secretary general of the CNDD-FDD was evacuated abroad

Reverien Ndikuriyo, secretary general of the CNDD-FDD (ruling party) suddenly fell ill on Thursday. From Ngozi (northern Burundi), he was transferred to Bujumbura (commercial capital), before being evacuated to Nairobi,

Politic

Burundi: IDHB notes a precarious lull and a fierce struggle at the top of the regime

The Initiative for Human Rights in Burundi, IDHB, has released its annual report describing a fierce struggle at the top of the Burundian administration which seems to hide a lull

Health

Burundi : blood is lacking at the regional blood transfusion center in the south

Health officials in the southern provinces of Burundi fear for patients lacking blood donations, including patients suffering from anemia. Health officials speak of a very alarming situation. INFO SOS Médias