Cibitoke: watu 15 walipatikana na ugongwa wa kipindipindu kwa kipindi cha chini ya wiki mbili eneo la Rugombo
Janga la kipindipindu linaripotiwa katika eneo la Mparambo tarafani Rugombo mkoa wa Cibitoke (kaskazini magharibi mwa Burundi) tangu wiki mbili zilizopita. Wagonjwa 15 walipatikana. Ukosefu wa maja safi ndio chanzo cha ugonjwa huo. Maafisa wa afya katika mkoa wa Cibitoke wanafahamisha kuwa hawajuwi ulikotoka ugonjwa huo. HABARI SOS Médias Burundi
Visa vya maradhi ya kipindipindu vinaripotiwa mnamo siku chache zilizopita katika eneo la mkoa wa Cibitoke kwenye mwambao wa mto wa Rusizi, unatofautisha nchi za Burundi na DRC. Angalau watu 15 waliopatikana na ugonjwa huo walipokelewa katika huduma ya dharura ya kituo cha afya cha Rugombo.
Wagonjwa wote kulingana na vyanzo katika utawala wanatoka katika kijiji cha Mparambo I tarafani Rugombo kwenye umbali wa kilometa kumi kutoka makao makuu ya mkoa.
Shirika la waganga wa msalaba mwekundu ambalo linatoa huduma zote lilikabidhi pia kituo hicho cha afya gari la wagonjwa kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa wagonjwa.
Shirika la msalaba mwekundu la Burundi na kikosi cha polisi cha kukinga majanga wanawajibika kwa kasi kunyunyizia dawa ndani ya majumba ambako wagonjwa wanaishi. Nyumba zote katika eneo hilo zimepewa huduma ya maji safi.
Regideso ( mamlaka ya umaa ya maji na umeme) inashiriki pia ili maji safi yapatikane. Eneo lililoathiriwa linakabiliwa na ukosefu wa huduma hiyo.
Viongozi wa afya mkoani Cibitoke wanafahamisha kuwa kampeni ya kuwahamasisha raia imeanza kwa ushirikiano na viongozi tawala.
” ni kutokana na uhaba wa maji safi ambapo ugonjwa huo uliripuka”, wanasema.
You might also like
Rumonge: at least 236 houses destroyed by torrential rains
This Monday, heavy rains fell in several villages in the Kizuka zone. It is in the district and province of Rumonge (Southwest Burundi). The provisional result given by local authorities
Rutana: mfungwa alifumaniwa akifanya mapenzi, Mwendeshamashtaka aomba pesa wafungwa
Wafungwa walilazimishwa kulipa kila mmoja franka elfu 20. Ni pesa iliyokusanywa ili kumlipa asivunje siri mwendeshamashtaka wa Rutana (kusini mashariki mwa Burundi). Mwendeshamashtaka alimufumania mfungwa mmoja akifanya mapenzi katika ofisi
Burundi : subsidized fertilizers now conditional on contour lines
SOS Médias Burundi Gitega, September 25, 2025 — Burundian Prime Minister Nestor Ntahontuye announced Thursday that the allocation of organo-mineral fertilizers will now be reserved for farmers who have traced
