Goma-Gavana mwanajeshi kwa wananchi: askali jeshi wa kikosi cha EAC sio maadui zetu

Goma-Gavana mwanajeshi kwa wananchi: askali jeshi wa kikosi cha EAC sio maadui zetu

Gavana wa kijeshi wa mkoa wa kivu kaskazini aliwaomba wananchi wakaazi wa mkoa huo kuacha kushambulia kwa maneno askali waliotumwa mashariki mwa DRC chini ya kikosi cha kikanda cha jumuiya ya Afrika mashariki (EAC). Wito huo umejumuishwa katika tangazo la ofisi ya luteni jemedali Constant Ndima la jumatano hii.

HABARI SOS Médias Burundi

Kulingana na tangazo hilo, wanajeshi waliotumwa katika mkoa wa kivu kaskazini walikuja kutekeleza makubaliano ya Luanda (Angola) , Nairobi (Kenya) na Addis-Abeba (Ethiopia). Ni makubaliano ambayo serikali ya Kongo ilihusika kwa lengo la kupata suluhu la mzozo unaoendelea mashariki mwa Kongo, alifahamisha luteni kanali Ndjike Kaiko Guillaume msemaji wa serikali ya Kivu kaskazini.

Katika tangazo hilo, serikali ya mkoa inadai kuwa kushambulia kwa maneno vikosi hivyo itawapelekea ” kuanguka katika mtego wa adui”.

” Kwa hiyo, serikali inakariri kuwa ilidhinisha vikosi hivyo vya kikanda kuingia “.

Tangu novemba 2022, kikosi cha kikanda cha EAC tayari kilikuwa kimetuma wanajeshi kutoka Kenya na Burundi mjini Goma. Wanajeshi pia kutoka Uganda na Sudan ya kusini wanasubiriwa.

Hivi karibuni, mandamano mengi dhidi ya kikosi hicho yaliandaliwa katika mji wa Goma ( makao makuu ya Kivu kaskazini) kwa ombi la makundi ya ushawishi na wanasiasa wanaodai kuwa kikosi hicho ” hakiwajibiki na kuegemea upande” kama Monusco ( ujumbe wa umoja wa mataifa nchini DRC) .

Previous Nduta (Tanzania) : kaburi labomorewa na viongozi kwa hoja tu ya kujengwa kwa simenti
Next Mahama (Rwanda) : mauwaji ya angalau wakimbizi nane kutoka Burundi yasababisha wasi wasi

You might also like

Security

Cibitoke: three illegal gold miners dead in a landslide

At least three illegal gold miners were killed in a landslide on the afternoon of Friday June 28 on the transverse road 7 of Rusororo hill. It is in the

Security

North Kivu: the populations victims of looting in the combat zones in the Masisi territory

During the clashes between the M23 rebels and the armed forces of the Democratic Republic of Congo, more than 800 cows were taken from the villages of Kaundu, Buhumba and

Human Rights

Cibitoke: four ladies killed the day before women’s day

Four women were killed and eight girls victims of rape at the start of the month dedicated to women in the communes of Rugombo, Murwi, Bukinanyana and Buganda, in Cibitoke