Goma-Gavana mwanajeshi kwa wananchi: askali jeshi wa kikosi cha EAC sio maadui zetu
Gavana wa kijeshi wa mkoa wa kivu kaskazini aliwaomba wananchi wakaazi wa mkoa huo kuacha kushambulia kwa maneno askali waliotumwa mashariki mwa DRC chini ya kikosi cha kikanda cha jumuiya ya Afrika mashariki (EAC). Wito huo umejumuishwa katika tangazo la ofisi ya luteni jemedali Constant Ndima la jumatano hii.
HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na tangazo hilo, wanajeshi waliotumwa katika mkoa wa kivu kaskazini walikuja kutekeleza makubaliano ya Luanda (Angola) , Nairobi (Kenya) na Addis-Abeba (Ethiopia). Ni makubaliano ambayo serikali ya Kongo ilihusika kwa lengo la kupata suluhu la mzozo unaoendelea mashariki mwa Kongo, alifahamisha luteni kanali Ndjike Kaiko Guillaume msemaji wa serikali ya Kivu kaskazini.
Katika tangazo hilo, serikali ya mkoa inadai kuwa kushambulia kwa maneno vikosi hivyo itawapelekea ” kuanguka katika mtego wa adui”.
” Kwa hiyo, serikali inakariri kuwa ilidhinisha vikosi hivyo vya kikanda kuingia “.
Tangu novemba 2022, kikosi cha kikanda cha EAC tayari kilikuwa kimetuma wanajeshi kutoka Kenya na Burundi mjini Goma. Wanajeshi pia kutoka Uganda na Sudan ya kusini wanasubiriwa.
Hivi karibuni, mandamano mengi dhidi ya kikosi hicho yaliandaliwa katika mji wa Goma ( makao makuu ya Kivu kaskazini) kwa ombi la makundi ya ushawishi na wanasiasa wanaodai kuwa kikosi hicho ” hakiwajibiki na kuegemea upande” kama Monusco ( ujumbe wa umoja wa mataifa nchini DRC) .
About author
You might also like
DRC: South Kivu teams up with the North to oppose the regional force
Rallies were held, on Tuesday, in several cities and entities of South Kivu, Eastern DRC to call for “a halt to all activity” to “ask for the departure of the
Bujumbura: the husband of the sister of the opponent Aimé Magera arrested like his wife
He was apprehended in unclear circumstances after receiving a call from an Imbonerakure (member of the CNDD-FDD youth league). He is reportedly detained in the same place as his wife.
North Kivu-Ituri: 30 ADF fighters killed
A total of 30 ADF (Allied Democratic Forces) rebels were killed not far from Boga in Irumu territory, Ituri province in eastern DRC. Colonel Mak Hazukay, spokesman for the joint