Kakuma (Kenya) : Zaidi ya watu 200 wanaotafuta hifadhi ya ukimbizi wakubaliwa
Zaidi ya watu 200 walipokelewa katika vituo viwili vya muda ndani ya kambi ya wakimbizi ya Kakuma kaskazini magharibi mwa Kenya mnamo siku zilizopita. Hayo ni wakati ambapo zaidi ya wakimbizi 3500 wa burundi wa kambi ya Kakuma wanataka kurejea katika nchi yao baada ya miaka kadhaa ya ukimbizi. HABARI SOS Médias Burundi
Ripoti ya shirika la HCR-Kenya inasema kuwa nchi hiyo inaendelea kuwapokea raia wa Burundi wanaotafuta hifadhi.
Kwa mfano, kamati ya wakimbizi na HCR inahakikisha kuwa zaidi ya watu 200 raia wa Burundi walipokelewa katika kipindi kisichozidi mwezi mmoja.
Msafara wa kwanza wa watu 60 ulifika mwanzoni mwa mwezi septemba. Msafara wa pili na tatu ulifika katika mwezi oktoba ukiwa na watu 70, shirika la HCR linasema.
Wakimbizi wanaowasili wanaundwa kwa sehemu kubwa na akinamama na watoto kulingana na viongozi wa kijamii.
” Wanakuja na ma basi ya uchukuzi. Tunawapokea akinamama na watoto. Wanatoka moja kwa moja Burundi, Rwanda, Tanzania na Uganda. Wanasema kuwa wanakimbia usalama mdogo na hali duni ya maisha katika kambi ndani ya nchi hizo jirani ya Kenya”, alibaini viongozi mmoja wa kijamii.
Kwa mjibu wa taarifa zetu, warundi hao kwa sasa wanapewa hifadhi katika vituo vya muda ndani ya kambi ya Kakuma wakisuburi faili zao zishughulikiwe ili wapate hifadhi ya ukimbizi.
” Vituo hivyo viwili vimezidiwa na idadi ya watu sababu mbali na Burundi, kuna pia raia wa somalia, sudani kusini na Ethipia.Tunaomba HCR iweze kuharakisha mchakato wa kuwapa hifadhi ya ukimbizi au kuandaa kituo kingine ili kuepuka majanga” alibaini kiongozi mmoja wa kijamii eneo la kakuma.
wakati huo huo, kambi inaorodhesha wakimbizi wa burundi wanaotaka kurudi makwao.
” Hakika ni hali ya kukanganya na hatuelewi kinachoendelea. Hapa tunawapokea warundi lakini wakati huo, orodha ya wanaotaka kurudi nchini inaendelea kuwa ndefu siku baada ya siku.Jana niliona kuwa wanakadiriwa 3500″ alifahamisha raia wa Burundi anayejitolea katika mmoja kati mashirika ya kihisani katika kambi ya Kakuma.
Kambi ya Kakuma inawapa hifadhi wakimbizi zaidi ya laki mbili wakiwemo warundi elfu 20.
You might also like
Nakivale (Uganda) : more than a thousand schoolchildren take the national exam
SOS Médias Burundi Nakivale, November 5, 2025 — In the Nakivale refugee camp, located in southwestern Uganda, education remains a major challenge for young refugees. Despite economic hardship, more than
Photo of the week : 1,150 Rwandan refugees repatriated in 48 hours
In the space of 48 hours, exactly 1,150 Rwandan refugees were repatriated from the eastern Democratic Republic of Congo to Rwanda. This large-scale operation was coordinated by the United Nations
Burundi : after nearly three years of waiting, Congolese refugees regain a single status
Hundreds of Congolese refugees living in Burundi have finally seen their administrative situation regularized, after years of stalemate caused by double registration in several countries. UNHCR-Burundi conducted a major clarification
