Rwanda-DRC: mwanajeshi wa Kongo wa pili kuuwawa na jeshi la Rwanda
Jeshi la Rwanda limefamisha kuwa limemuuwa mwanajeshi wa Kongo jumamosi tarehe 19 novemba. Jeshi linaendelea kuwa amevuka mpaka na kuanza kuwapiga risasi wanajeshi wake. HABARI SOS Médias Burundi
Ni kupitia tangazo ambapo jeshi la Rwanda limetangaza kifo cha mwanajeshi huyo wa FARDC (Jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) .
Tamko hilo linasema kuwa alikuwa akipiga risasi kwenye ngome za jeshi la Rwanda wakati alipopigwa risasi na kufariki.
Kisa hicho kimetokea katika eneo la mpakani linalojulikana kama “petite barrière”. Ni kati ya wilaya ya Rubavu (magharibi mwa Rwanda) na mji wa Goma (makao makuu ya mkoa wa Kivu ya kaskazini) mashariki mwa DRC.
Viongozi wa Kongo hawajasema lolote kuhusu kisa hicho.
Mwanzoni mwa mwezi juni mwaka huu, mwanajeshi mwingine wa Kongo aliuwawa na polisi wa Rwanda kwenye kizuizi hicho wakati akiwapiga risasi maafisa wa idara ya uhamiaji na raia wa kawaida, kwa mjibu wa jeshi la Rwanda.
Tukio hilo kilisababisha malalamiko makubwa ndani ya miji ya mashariki mwa Kongo. Mashirika ya kiraia na makundi mengine ya shinikizo yaliomba viongozi wa Kongo ” kufunga mipaka yake na Rwanda “.
Katika visa hivyo viwili, jeshi la Rwanda linafahamisha kuwa lilitoa taarifa kwa shirika la CIRGL (kongamano la kitaifa katika kanda la maziwa makuu)
You might also like
Mutaho: the post office manager killed
Emmanuel Ndayikengurutse was killed early in the afternoon. Perpetrators of the crime have been arrested. He was the local manager of the national post of Burundi. INFO SOS Médias Burundi
Cibitoke : Rwandan rebels killed in the intelligence service cell
Several Rwandan FLN rebels, incarcerated in the dungeon of the national intelligence service in Cibitoke (northwest Burundi), were killed. Sources within the police affirm that their bodies were immediately driven
Rwanda-DRC: DRC once again accuses Rwanda of supporting the M23 (press release)
The Congolese government has once again accused Rwanda of supporting the March 23 Movement (M23), a rebel movement fighting the government of the Democratic Republic of Congo (DRC), a statement
