Nyarugusu (Tanzania): wasi wasi kufuatia mvutano kati mashirika mawili ya misaada
Katika kambi ya Nyarugusu, mashirika mawili ya misaada yanashindana katika sekta ya elimu. Mashirika hayo ni pamoja na “Save the children” na “IRC”. Kama madhara, shule hazikufunguliwa jumatatu hii. HABARI SOS Médias Burundi
Mashirika hayo mawili yanataka kuhudumu katika sekta ya elimu katika kambi za wakimbizi nchini Tanzania.Kawaida shirika la Save the children ndilo linahudumu katika sekta hiyo.
” Kwa wakati huu, mashirika mengine yaliachia nafasi shirika la Danish Refugee Council (RDC), shirika jingine la International Rescue Commitee linataka kupewa nafasi katika sekta ya elimu. Kwa hiyo mvutano unaripotiwa kati ya mashirika hayo mawili ya misaada. Tuna pia hofu kuhusiana na mishahara yetu”. anaeleza mwalimu mmoja katika kambi ya Nyarugusu.
Madhara ya mzozo huo ni shule kutofunguliwa jumatatu hii. Wanafunzi wamefukuzwa bila kuambiwa lini watarudi shuleni.
” Wanafunzi wetu wamekwenda sheleni lakini waalimu hawakuwepo. Waalimu wanaotoka nje ya kambi hawakuruhusiwa kuingia kambini. Kwa hiyo hatungetoa visomo wakati wenzetu wa Tanzania wakiwa wameshinda. Tunaomba swala hilo lijadiliwa kwa ngazi ya juu ili visomo katika awamu ya pili ya mwaka wa shule iweze kuendelea kama kawaida “, waalimu walielezea wakimbizi.
Kwenye kambi ya Nyarugusu, shule tano ziko chini ya uangalizi wa shirika la Save the children tangu miaka 7 iliyopita.
Katika kambi mbali mbali, urasibu wa mashirika ya misaada unahusisha HCR na serikali ya Tanzania. Wazazi wanaomba tatizo hilo liondolewe ili visomo visije kusimama kwa muda mrefu hususan katika darasa za mtihani na zile za kumalizia kidato.
Tatizo hilo linaripotiwa pia katika ya Nduta hata kama visomo bado kusimama.
Kambi hizo mbili zinajumulisha zaidi ya wakimbizi kutoka Burundi laki moja na elfu 26.
You might also like
Four boys rescued from human trafficking between Burundi and Tanzania
SOS Médias BurundiRumonge, October 3, 2025 — Four teenagers from southern Burundi were repatriated on Monday after falling victims to a human trafficking network operating between Burundi and Tanzania. These
Bururi: four people from the same family in detention
Four people belonging to the same family have been detained since Christmas night in police cells in Bururi (southern Burundi). Three of them are suspected of having tried to free
Musasa : a refugee camp without water for six months, the humanitarian crisis worsens
SOS Médias Burundi Kiremba, June 11, 2026 – The humanitarian situation is becoming increasingly worrying in the Musasa refugee camp, in Kiremba district, Butanyerera province, northern Burundi, where more than
