Cibitoke: zaidi ya vitenge 300 vilikamatwa kwa mfuasi wa CNDD-FDD eneo la Buganda

Cibitoke: zaidi ya vitenge 300 vilikamatwa kwa mfuasi wa CNDD-FDD eneo la Buganda

Zaidi ya vitenge 300 kutoka jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo vilikamatwa na polisi kwa mfuasi wa chama tawala mwenye ushawishi. Msako ulifanyika eneo la Nyamitanga kijiji cha Ndava tarafani Buganda (mkoa wa Cibitoke kaskazini magharibi mwa Burundi). Ilikuwa tarehe 25 oktoba.Wakaazi wanaomba sheria itumike. Idara ya sheria mkoani Cibitoke inafahamisha kuwa taarifa imewafikia na kuzidi kuwa uchunguzi umeanzishwa. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa jumla vitenge 322 vilikamatwa jumanne tarehe 25 kwake Adeline Ingabire mjumbe wa baraza la tarafa ya Buganda ambaye ni kutoka chama tawala na yuko kwenye orodha ya wabunge waliochaguliwa katika mkoa wa Cibitoke.

Mke huyo wa mshahuri wa zamani wa balozi wa Burundi mjini Brussels ni mmoja kati ya viongozi wakuu wa chama cha CNDD-FDD. Anajulikana kama mwanamke mwenye ushawishi ndani ya chama tawala.

” Sio kisa cha kwanza. Alituhumiwa mara nyingi kuhusika na biashara haramu hasa biashara ya vitenge”, chanzo katika polisi kwenye makao makuu ya mkoa wa Cibitoke kilieleza.
Mwanamke huyo aliwahi kuitishwa katika mwaka wa 2021 bila hata hivyo kusikitika wakati akijaribu kuingiza nchini Burundi bidhaa ya vitenge pasina kulipa ushuru kwenye mamlaka ya ushuru na kodi OBR nchini kupitia mpaka kati ya Burundi na Kongo kwenye mto Rusizi.

Mfanyabiashara mmoja anahakikisha kuwa mtuhumiwa huyo alinufaika kwa kipindi kirefu na ushirikiano wa vigogo wa chama tawala.Anazidi kuwa mtuhumiwa huyo hataguswa.

“Maajabu zaidi, vitenge hivyo vitarudishwa kwake haraka wakati ambapo vimekamatwa na OBR,” analalamika mfanyabiashara huyo.

Habari hiyo inathibitishwa na polisi ya Cibitoke ambayo inazidi kuwa vitenge hivyo vilikabidhiwa vyombo vya sheria.
Akiulizwa juu ya mkasa huo, Mwendeshamashtaka wa jamuhuri mkoani Cibitoke amefahamisha kuwa uchunguzi umeanzishwa. Anaomba watu kusubiri kwa utulivu matokeo ya uchunguzi huo.
Amejizuia kusema lolote kuhusiana na swala la kwa nini mtuhumiwa hakusimamishwa wakati alifumaniwa na biashara haramu.

Previous Mugamba: torrential rains caused several damages
Next Rutana: mfuasi mwenye ushawishi wa chama cha CNDD-FDD akungwa mwaka mmoja jela

You might also like

Economy

Price surge in Cibitoke : an end-of-Ramadan celebration weighed down by the high cost of living

While Muslims in Cibitoke (northwestern Burundi) celebrated the end of Ramadan on March 30, the widespread rise in the prices of basic necessities is weighing heavily on households. Rice, beans,

Governance

Burundi : 18 tons of coffee seized in Mpanda, a trader detained for two weeks

SOS Médias Burundi Mpanda, June 5, 2026 – A trader from the Ruce zone of ​​Mpanda district, Bujumbura province, in western Burundi, has been detained since May 21, 2026, in

Economy

Musigati: a decision to destroy 50 sugar-cane-hectares

The administration issued a decision banning to grow sugar cane in the Musigati commune’s marshes in Bubanza province (western Burundi). The crop must be substituted with other food crops, according