Rwanda-DRC: mwanajeshi wa Kongo wa pili kuuwawa na jeshi la Rwanda
Jeshi la Rwanda limefamisha kuwa limemuuwa mwanajeshi wa Kongo jumamosi tarehe 19 novemba. Jeshi linaendelea kuwa amevuka mpaka na kuanza kuwapiga risasi wanajeshi wake. HABARI SOS Médias Burundi
Ni kupitia tangazo ambapo jeshi la Rwanda limetangaza kifo cha mwanajeshi huyo wa FARDC (Jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) .
Tamko hilo linasema kuwa alikuwa akipiga risasi kwenye ngome za jeshi la Rwanda wakati alipopigwa risasi na kufariki.
Kisa hicho kimetokea katika eneo la mpakani linalojulikana kama “petite barrière”. Ni kati ya wilaya ya Rubavu (magharibi mwa Rwanda) na mji wa Goma (makao makuu ya mkoa wa Kivu ya kaskazini) mashariki mwa DRC.
Viongozi wa Kongo hawajasema lolote kuhusu kisa hicho.
Mwanzoni mwa mwezi juni mwaka huu, mwanajeshi mwingine wa Kongo aliuwawa na polisi wa Rwanda kwenye kizuizi hicho wakati akiwapiga risasi maafisa wa idara ya uhamiaji na raia wa kawaida, kwa mjibu wa jeshi la Rwanda.
Tukio hilo kilisababisha malalamiko makubwa ndani ya miji ya mashariki mwa Kongo. Mashirika ya kiraia na makundi mengine ya shinikizo yaliomba viongozi wa Kongo ” kufunga mipaka yake na Rwanda “.
Katika visa hivyo viwili, jeshi la Rwanda linafahamisha kuwa lilitoa taarifa kwa shirika la CIRGL (kongamano la kitaifa katika kanda la maziwa makuu)
You might also like
Murwi : a septuagenarian beheaded
Samuel Kabuye (71 years old) was killed on the morning of this Wednesday. The murder took place in Remera village in district in Cibitoke province (northwest Burundi). Six suspects were
Beni : zaidi ya watu 70 wauwawa katika kipindi cha siku 6
Zaidi ya watu 70 waliuwawa katika kipindi cha siku sita zilizopita katika wilaya ya Beni , Kivu kaskazini katika vijiji mbali mbali mashariki mwa DRC. Waliotekeleza mauwaji hayo ni waasi
Goma: large-scale protests
The city of Goma (capital of North Kivu, eastern DRC) woke up in great tension on Monday morning following a protest against the regional force of the EAC. The protesters
