Burundi : kitita cha milioni 21 chatolewa na benki ya afrika ya maendeleo kwa ajili ya kuendeleza sekta ya kilimo
Mikoa ya kaskazini mashariki mwa Burundi ambayo ni : Ngozi, Kirundo na Muyinga itanufaika na mradi hui kwa kutengeneza mabonde ya mito mingi. Lengo ni kuongeza mavuno ya kilimo kwa ajili ya kukabiliana na usalama mdogo wa chakula. HABARI SOS Médias Burundi
Mradi huo ulizinduliwa alhamisi iliyopita katika mkoa wa Kirundo kaskazini mwa nchi. unahusika na kuongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo na ufugaji.
Dola za kimarekani milioni 21 zilitolewa kwa serikali ya Burundi na banki ya afrika kwa ajili ya maendeleo (BAD).
Mjumbe wa BAD katika nchi hiyo ndogo ya afrika mashariki alifahamisha kuwa “Tunashirikiana na serikali katika mipango yake”.
Mradi huo wa kuunga mkono maendeleo endelevu ya kilimo na ufugaji nchini Burundi ( PADCAE_B) utatekelezwa katika mikoa ya Ngozi, Kirundo na Muyinga.
Utasaidia katika kukabiliana ya uhaba wa chakula na kuendeleza ajira kwa vijana na kutekeleza kilimo cha uhakika.
Madhumuni kulingana na mjumbe wa BAD ” kuhakikisha kuwa watu milioni tatu katika maeneo hayo matatu yaliyochaguliwa wamepata uwezo wa kuzalisha vya kutosha”.
Waziri wa kilimo Sanctus Niragira alifahamisha kuwa mradi huo ulianzishwa kwa lengo la kupata suluhu la tatizo la usalama mdogo wa chakula nchini Burundi “.
Mradi huo wa miaka minne utatamatishwa mwishoni mwa juni 2026.
Shughuli zinazopangwa kufanyika ni pamoja na kutengeneza katika mfumo wa kisasa bonde la mto Nyamuswaga linalogusa mikoa ya Muyinga na Ngozi, bonde la Nyamabuno linalogusa mikoa ya Muyinga na Kirundo. Mito ya Rucikiri mkoani Muyinga, Ruyongwe katika mikoa ya Kirundo -Ngozi na Muyinga pamoja pia na Ruganirwa unaopatikana katika mkoa wa Kirundo utahusika pia.
Waziri Niragira aliwaomba raia wanaolengwa na mradi huo ” kujari uwezo wanaopewa kwa ajili ya kuendeleza mradi huo”.
You might also like
Bujumbura : CNEB warns of socio-economic challenges and reiterates the role of churches as Easter and elections approach
SOS Médias BurundiBujumbura, April 19, 2025 – With Easter approaching and in a tense political and economic context, the National Council of Churches of Burundi (CNEB) expresses its concern about
DRC: jamii ya kimataifa yafumbia macho vurugu zinazowakabili wananchi wa Kongo (Baba mtakatifu François)
Baba mtakatifu François jumanne hii tarehe 31 januari alianza rasmi ziara ya siku sita barani Afrika. Anataraji kufanya siku nne nchini DRC na kumalizia siku zinazosalia nchini Sudan kusini. Alilaani
Mugina: two people dead and three others injured following torrential rains
Two people died, three others seriously injured and several houses and fields washed away by heavy rain mixed with hail and violent winds on the hills of Kagurutsi and Nyamihana
