Makamba : chumba cha kuhifadhi maiti hakifanyi kazi kwa takriban mwaka mmoja sasa
Kwa mjibu wa wafanyakazi kwenye hospitali hiyo ya Makamba ( kusini mwa Burundi) pamoja na familia zilizokosa watu, chumba cha kuhifadhi maiti sasa ni takriban mwaka mmoja kikiwa hakifanyi kazi. Baadhi ya familia wanalalamika kuwa miili ya watu wao inaharibika kabla ya kuzikwa. Hata hivyo bili ya kuhifadhi maiti ndani ya chumba hicho inazidi kutolewa, ni franka elfu 15 kwa kila siku wakati ambapo chumba hicho hakifanyi kazi. Wakaazi wanaomba kitengenezwe mara moja. HABARI SOS Médias Burundi
Familia moja inafahamisha kuwa ilipata matatizo katika mazishi ya mmoja kati ya wajumbe wake aliyefariki baada ya siku nne muili wake ukiwa ndani ya chumba cha hospitali hiyo cha kuhifadhi maiti.
Wanaeleza kuwa ” hatukuweza kuweka muili ndani ya sanduku sababu maiti ilikuwa imeharibika sana”.
Familia nyingi zinalalamika kupeleka miili ya wajumbe wao waliofariki katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali za Bururi na Rutana ( Kusini mashariki mwa Burundi).
” Mchakato huo unatugharimu pesa nyinshi kwa kukodi gari la kubeba maiti safari ya kwenda na kurudi na kujumulisha pia gharama za chumba hicho”, wanalaani familia hizo.
Taarifa hizo zinahakikishwa na wafanyakazi kwenye kituo hicho cha afya.
Viongozi wa hospitali hiyo hadi sasa bado hawajapata suluhu la tatizo hilo.
Wafanyakazi kwenye hospitali hiyo wanadai kuwa ” ni aibu kwa hospitali kuu ya mkoa inayowapokea wagonjwa kutoka mkoa wote”.
Wanajiuliza sababu zinazopelekea viongozi wa hospitali hiyo kuacha kutengenezesha chumba hicho wakati ambapo hospitali hiyo ni moja kati ya zile zinazoomba gharama kubwa ya kuweka maiti ndani ya chumba cha kuhifadhi maiti.
Familia za wahanga na wafanyakazi wa hospitali ya Makamba wanaomba viongozi wakuu katika sekta ya afya kushinikiza ili viongozi wa kituo hicho cha afya watengenezeshe chumba hicho.
Wiki iliyopita, walikuwa walionekana kuanza kutengenezesha chumba hicho cha kuhifadhi maiti wakati wa ziara ya waziri wa afya katika mkoa huo lakini kazi zilisimama kwa mjibu wa mashahidi.
You might also like
Photo of the week : Rwandan FLN rebels reported in some public places in Mabayi, the administration decides to close them
The measure announcing the closure of all activities in the center of Kivogero frequented by rebels speaking Kinyarwanda settled in the Kibira natural reserve was taken by the administrator of
Burundi : it is normal that Burundian soldiers are killed in the DRC (President Neva)
President Neva announced Friday that “the M23 is waging psychological warfare” and affirmed that it is normal for soldiers of the FDNB (Burundi National Defense Force) to be killed in
Bujumbura attack : Burundian authorities took official stock and accused Rwanda again
After Friday’s early evening grenade attack on a public transport bus parking lot in the commercial city Bujumbura, Burundian authorities reported 38 injured, including 5 seriously. A spokesperson for the
