Makamba : chumba cha kuhifadhi maiti hakifanyi kazi kwa takriban mwaka mmoja sasa
Kwa mjibu wa wafanyakazi kwenye hospitali hiyo ya Makamba ( kusini mwa Burundi) pamoja na familia zilizokosa watu, chumba cha kuhifadhi maiti sasa ni takriban mwaka mmoja kikiwa hakifanyi kazi. Baadhi ya familia wanalalamika kuwa miili ya watu wao inaharibika kabla ya kuzikwa. Hata hivyo bili ya kuhifadhi maiti ndani ya chumba hicho inazidi kutolewa, ni franka elfu 15 kwa kila siku wakati ambapo chumba hicho hakifanyi kazi. Wakaazi wanaomba kitengenezwe mara moja. HABARI SOS Médias Burundi
Familia moja inafahamisha kuwa ilipata matatizo katika mazishi ya mmoja kati ya wajumbe wake aliyefariki baada ya siku nne muili wake ukiwa ndani ya chumba cha hospitali hiyo cha kuhifadhi maiti.
Wanaeleza kuwa ” hatukuweza kuweka muili ndani ya sanduku sababu maiti ilikuwa imeharibika sana”.
Familia nyingi zinalalamika kupeleka miili ya wajumbe wao waliofariki katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali za Bururi na Rutana ( Kusini mashariki mwa Burundi).
” Mchakato huo unatugharimu pesa nyinshi kwa kukodi gari la kubeba maiti safari ya kwenda na kurudi na kujumulisha pia gharama za chumba hicho”, wanalaani familia hizo.
Taarifa hizo zinahakikishwa na wafanyakazi kwenye kituo hicho cha afya.
Viongozi wa hospitali hiyo hadi sasa bado hawajapata suluhu la tatizo hilo.
Wafanyakazi kwenye hospitali hiyo wanadai kuwa ” ni aibu kwa hospitali kuu ya mkoa inayowapokea wagonjwa kutoka mkoa wote”.
Wanajiuliza sababu zinazopelekea viongozi wa hospitali hiyo kuacha kutengenezesha chumba hicho wakati ambapo hospitali hiyo ni moja kati ya zile zinazoomba gharama kubwa ya kuweka maiti ndani ya chumba cha kuhifadhi maiti.
Familia za wahanga na wafanyakazi wa hospitali ya Makamba wanaomba viongozi wakuu katika sekta ya afya kushinikiza ili viongozi wa kituo hicho cha afya watengenezeshe chumba hicho.
Wiki iliyopita, walikuwa walionekana kuanza kutengenezesha chumba hicho cha kuhifadhi maiti wakati wa ziara ya waziri wa afya katika mkoa huo lakini kazi zilisimama kwa mjibu wa mashahidi.
You might also like
Rwanda: wakimbizi wa Kongo walalamika mbele ya ubalozi tofauti mjini Kigali
Wawakilishi wa zaidi ya wakimbizi 70.000 kutoka Kongo wanaopewa hifadhi nchini Rwanda waliwasilisha waraka kwenye balozi tofauti mjini Kigali jumatatu hii tarehe 23 januari ili kufahamisha jamii ya kimataifa kusaidia
Burundi : opposition boycott and tensions surrounding the electoral process ahead of 2027
SOS Médias Burundi Bujumbura, May 9, 2026 — In Bujumbura, Burundi’s commercial capital and home to UN agencies and the central government, the electoral process leading up to the 2027
Gitega: two unsolved murders in the districts of Gishubi and Mutaho
Two corpses were found in the districts of Gishubi and Mutaho, in the province of Gitega (central Burundi). It is the corpse of an ex-Fab (a retired soldier from the
