Mahama (Rwanda) : mkimbizi wa Burundi afariki dunia baada ya kupigwa na wakimbizi kutoka Kongo
Emmanuel Ruremesha aliuwawa jumanne hii tarehe 28 februari. Alifariki kutokana na vipigo alivyofanyiwa wakati wa ugomvi na raia wa Kongo usiku wa kuamkia jumanne hii. Polisi tayari ilikamata watu kadhaa kwa sababu za uchunguzi. HABARI SOS Médias Burundi
Ugomvi iliyosababisha kifo cha Ruremesha ulifanyika katika mgahawa wa pombe ndani ya kambi ya Mahama.
” Alipigwa vibaya hadi damu kutililika mdomoni na puwani” mashahidi walieleza.
Licha ya kupelekwa haraka kwenye hospitali ya ” Save the Children” katika zone ya Mahama ll, alifariki dunia siku moja badaye vyanzo vyetu viliendelea kueleza.
Muili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Kirehe kwa vile wahudumu wa afya ndani ya kambi wakiwa hawana huduma ya kufanya mazishi.
Baada ya tukio hilo, polisi iliingilia kati na kuwasimamisha watu kadhaa kwa lengo la kufanya uchunguzi.
Watu wa karibu na muhanga, wanaomba muhusika wa mauwaji hayo aweze kuadhibiwa kwa mjibu wa sheria.
Tangu tukio hilo, polisi ilizidisha doria katika eneo la tukio. Wanahofu kuwa warundi wanaweza kulipiza kisasi dhidi ya raia wa Kongo.
Amri ya kufunga mapema mgahawa ilitolewa kwa mmiliki wake.
Amekuwa mkimbizi wa Burundi wa nne kuuwawa katika ukanda huo katika mwezi huu. Wakimbizi wengine wa Burundi waliuwawa katika kambi ya Nduta nchini Tanzania na mwingine katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwezi februari ulioyopita.
You might also like
Lusenda: Burundian refugees asked not to leave the camp
It is the national commission for refugees in the Congo that wants the refugees to stay inside the camp as it feels not wise for the refugees to go out
Meheba (Zambia) : worrying increase in food prices on markets
Refugees in the Meheba camp in Zambia are alarmed by the increase considered exorbitant in prices on the camp markets. The increase concerns all basic foodstuffs and is partly due
Buganda : the Burundian army receives Congolese and Rwandan fighters and militiamen fleeing defeats against the M23
SOS Médias Burundi Buganda, December 11, 2025 — Between December 7 and 10, more than 2,000 aCongolese and Rwandan afighters and militiamen, fleeing defeats against the M23 rebels, were received
