Mahama (Rwanda) : mkimbizi wa Burundi afariki dunia baada ya kupigwa na wakimbizi kutoka Kongo
Emmanuel Ruremesha aliuwawa jumanne hii tarehe 28 februari. Alifariki kutokana na vipigo alivyofanyiwa wakati wa ugomvi na raia wa Kongo usiku wa kuamkia jumanne hii. Polisi tayari ilikamata watu kadhaa kwa sababu za uchunguzi. HABARI SOS Médias Burundi
Ugomvi iliyosababisha kifo cha Ruremesha ulifanyika katika mgahawa wa pombe ndani ya kambi ya Mahama.
” Alipigwa vibaya hadi damu kutililika mdomoni na puwani” mashahidi walieleza.
Licha ya kupelekwa haraka kwenye hospitali ya ” Save the Children” katika zone ya Mahama ll, alifariki dunia siku moja badaye vyanzo vyetu viliendelea kueleza.
Muili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Kirehe kwa vile wahudumu wa afya ndani ya kambi wakiwa hawana huduma ya kufanya mazishi.
Baada ya tukio hilo, polisi iliingilia kati na kuwasimamisha watu kadhaa kwa lengo la kufanya uchunguzi.
Watu wa karibu na muhanga, wanaomba muhusika wa mauwaji hayo aweze kuadhibiwa kwa mjibu wa sheria.
Tangu tukio hilo, polisi ilizidisha doria katika eneo la tukio. Wanahofu kuwa warundi wanaweza kulipiza kisasi dhidi ya raia wa Kongo.
Amri ya kufunga mapema mgahawa ilitolewa kwa mmiliki wake.
Amekuwa mkimbizi wa Burundi wa nne kuuwawa katika ukanda huo katika mwezi huu. Wakimbizi wengine wa Burundi waliuwawa katika kambi ya Nduta nchini Tanzania na mwingine katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwezi februari ulioyopita.
You might also like
Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC
Wanajeshi hao watatu waliuwawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na kundi la silaha la Twirwaneho linaloundwa na vijana wa jamii ya Banyamulenge, jumanne hii. HABARI SOS Médias Burundi
Tanzania : Burundian authorities want to repatriate refugees at all costs
A Burundian-Tanzanian delegation visited two Burundian refugee camps in Nduta and Nyarugusu this week. The message was unique : return before December 2024. However, most of those concerned do not
Ituri : nearly 30 ADF attackers killed, others captured and hostages released, according to the army
The Congolese army has taken stock of its operations during the month of January 2023 in Ituri province (eastern DRC). It claims to have killed 28 and captured 14 ADF
