Nyarugusu : yafungwa maduka ya dawa yasiyojulikana

Nyarugusu : yafungwa maduka ya dawa yasiyojulikana

Uwindaji wa wamiliki wa maduka ya dawa yasiyokuwa halali ulianzishwa ndani ya Nyarugusu. Shirika la Medical Team International linalohusika na sekta ya afya lina mpango wa kukataza tabia ya kujitibu na kujipangia dawa. HABARI SOS médias Burundi

Polisi, watu wanaojitolea, viongozi tawala pamoja na wahudumu walijumulishwa kuwahamasisha watu kuachana na tabia ya kujitibu wenyewe. Maduka na vibanda ambako dawa hununuliwa yalifichuliwa na kufungwa.

” Kisa cha kuchukulia mfano huo ni duka la dawa kubwa katika zone 9. Lilikuwa kwenye makaazi ya mkimbizi mmoja kutoka Burundi. Polisi imechukuwa madawa yote. Mumiliki wa duka hilo na mtumishi wamekamatwa. Nyumba iliyochukuliwa kama duka la dawa imefungwa” amethibitisha mkaazi wa zone hiyo.

Maduka ya dawa yamechukuliwa kama mahala pa kutibu na kupewa huduma za awali.

” Tulishuhudia kwa mfano vitongi vilivyokuwa vikiuzishwa karibu na nafaka za chakula, na watu wanaonunua dawa bila kuandikwa na muganga, etc…..Baya zaidi tulimukuta mgonjwa akipewa dawa kupitia serimu kati ya moja kati ya maduka ya madawa haliyofungwa. “Ni hali isoyovumilika ” walifafanua wahudumu wa shirika la Medical Team International.

Wito ulitolewa kwa kila mkimbizi anayejihisi vibaya kujielekeza kwenye kituo cha afya halali.

MTI hivi karibu ilichukuwa nafasi ya Croix Rouge katika sekta ya afya. Shirika hilo linataka kuleta mabadiliko ambayo kulingana na shirika ni kuongeza ubora wa huduma na kuhakikisha uheshimishwaji wa haki ya afya kwa kila mkimbizi.

Kambi hiyo inawapa hifadhi wakimbizi zaidi ya laki moja na elfu 10 wakiwemo warundi elfu 50, wanaosalia wakiwa wenye asili ya Kongo.

Previous Faili-Ecocash: Hali inazidi kuwa mbaya zaidi
Next DRC: jamii ya kimataifa yafumbia macho vurugu zinazowakabili wananchi wa Kongo (Baba mtakatifu François)

You might also like

Health

Mpanda : an unknown illness under surveillance; initial analyses rule out major hemorrhagic fevers

SOS Médias Burundi Mpanda, April 13, 2026 — An as-yet-unidentified illness, responsible for several cases and deaths in the Mpanda district, has been mobilizing Burundian health authorities for several days.

Health

Burundi : an unknown disease kills two people in Makamba, the population on alert

SOS Médias Burundi Burunga, July 5, 2025 – A mysterious disease has killed two people in Makamba district, now part of Burunga province, in southern Burundi. Health authorities are trying

Human Rights

Geneva : the term of the UN Special Rapporteur on the situation of human rights in Burundi renewed

The vote took place on Thursday. Of the 47 states that make up the Council, 22 voted in favor of the reappointment of Fortuné Gaétan Zongo. Burundian authorities had not