Nyarugusu : yafungwa maduka ya dawa yasiyojulikana

Nyarugusu : yafungwa maduka ya dawa yasiyojulikana

Uwindaji wa wamiliki wa maduka ya dawa yasiyokuwa halali ulianzishwa ndani ya Nyarugusu. Shirika la Medical Team International linalohusika na sekta ya afya lina mpango wa kukataza tabia ya kujitibu na kujipangia dawa. HABARI SOS médias Burundi

Polisi, watu wanaojitolea, viongozi tawala pamoja na wahudumu walijumulishwa kuwahamasisha watu kuachana na tabia ya kujitibu wenyewe. Maduka na vibanda ambako dawa hununuliwa yalifichuliwa na kufungwa.

” Kisa cha kuchukulia mfano huo ni duka la dawa kubwa katika zone 9. Lilikuwa kwenye makaazi ya mkimbizi mmoja kutoka Burundi. Polisi imechukuwa madawa yote. Mumiliki wa duka hilo na mtumishi wamekamatwa. Nyumba iliyochukuliwa kama duka la dawa imefungwa” amethibitisha mkaazi wa zone hiyo.

Maduka ya dawa yamechukuliwa kama mahala pa kutibu na kupewa huduma za awali.

” Tulishuhudia kwa mfano vitongi vilivyokuwa vikiuzishwa karibu na nafaka za chakula, na watu wanaonunua dawa bila kuandikwa na muganga, etc…..Baya zaidi tulimukuta mgonjwa akipewa dawa kupitia serimu kati ya moja kati ya maduka ya madawa haliyofungwa. “Ni hali isoyovumilika ” walifafanua wahudumu wa shirika la Medical Team International.

Wito ulitolewa kwa kila mkimbizi anayejihisi vibaya kujielekeza kwenye kituo cha afya halali.

MTI hivi karibu ilichukuwa nafasi ya Croix Rouge katika sekta ya afya. Shirika hilo linataka kuleta mabadiliko ambayo kulingana na shirika ni kuongeza ubora wa huduma na kuhakikisha uheshimishwaji wa haki ya afya kwa kila mkimbizi.

Kambi hiyo inawapa hifadhi wakimbizi zaidi ya laki moja na elfu 10 wakiwemo warundi elfu 50, wanaosalia wakiwa wenye asili ya Kongo.

Previous Faili-Ecocash: Hali inazidi kuwa mbaya zaidi
Next DRC: jamii ya kimataifa yafumbia macho vurugu zinazowakabili wananchi wa Kongo (Baba mtakatifu François)

You might also like

Refugees

South Kivu : Burundian Tutsi refugees targeted by ethnic hatred and authorities’ inaction

SOS Médias Burundi In the Mulongwe and Lusenda camps in South Kivu, eastern Congo, thousands of Burundian Tutsi refugees live under constant threat. Discrimination, violence, and deprivation : they accuse

Society

Covid-19 : more than 200 cases detected

A strong spread of the Covid-19 pandemic has been reported in Bururi province in southern Burundi. At least 172 cases have been detected in this southern province of the country

Refugees

Photo of the week : more than 8,000 Burundians, including former returnees, requested asylum in the DRC in two months

According to figures provided by the National Commission for Refugees in Uvira in the province from South Kivu (eastern DRC), eight thousand two hundred Burundians were registered in less than