Minembwe : kundi la Mai Mai limemuuwa mzee mmoja na kupora ng’ombe 150
Ndagara Buhimba (Miaka 80) aliuwawa siku ya jumatatu alasiri. Kundi la Mai Mai lilirejuhi pia watu 2 na kuiba ng’ombe 150. HABARI ya SOSMedias Burundi
Muhanga alikuwa katika malisho yaliyo katika eneo la Monyi wakati waasi wa Mai Mai waliopomuuwa kulinga na mashahidi.Ni katika kanda ya Minembwe wilaya ya Fizi katika mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.
Kifo cha mzee huyo kutoka jamii ya Banyamulenge kinathibitishwa na familia yake.
” Asubuhi hii ndipo muili wake umepatikana.Ni vitendo vya kinyama vinavyofanyika hapa. Watu wanauwawa kama wanyama wanachinjwa”, amelalamika mkaazi mmoja.
Vyanzo sehemu hiyo vinahakikisha kuwa watu wengine wawili walijeruhiwa wakati wa shambulio hilo ‘a ng’ombe 150 kuibiwa.
Msemaji wa kundi la Mai Mai hakuwa karibu ili aweze kujieleza juu ya malalamiko hayo. Wakuu wa jeshi na viongozi tawala pia hawajasema lolote.
Siku ya jumapili, kijana mdogo aliuwawa kwa kukatwa na panga na askali wa jeshi la FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo ) katika eneo hilo la Minembwe , kisa ambacho kilisababisha mandamano katika shule zote ijumatatu eneo la Minembwe.
Wakaazi wa eneo la Minembwe ambao wengi wao ni kutoka jamii ya Banyamulenge wanalituhumu jeshi la Kongo kutuwahami wakati wakilengwa na mashambulizi ya makundi ya silaha.
Ni tangu miaka mitano tukiuwawa bila hata hivo jeshi la FARDC kuingilia kati ili kutulinda wakati ambapo tuko raia wa Kongo ” analalamika diwani mmoja
You might also like
DRC : more than 1,800 children were recruited into armed groups in 2023 (UN)
At least 1,861 children, 1,535 boys and 326 girls were recruited and used by different local and foreign armed groups in the eastern Democratic Republic of Congo between January and
Goma: burial on government orders of more than forty bodies despite opposition from families and civil society
At least 40 bodies were buried on Monday September 18, 2023 on the orders of the governor of the North Kivu province in the east of the Democratic Republic of
Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali
Lionel Nzoyisaba alikuwa akijulikana kama mwizi tarafani Mpanda mkoa wa Bubanza. Alikuwa akiiba simu katika maduka eneo hilo. Usiku wa kuamkia tarehe mosi disemba, Nzoyisaba alisimamishwa na vijana Imbonerakure akitoka
