Nyarugusu (Tanzania): wasi wasi kufuatia mvutano kati mashirika mawili ya misaada
Katika kambi ya Nyarugusu, mashirika mawili ya misaada yanashindana katika sekta ya elimu. Mashirika hayo ni pamoja na “Save the children” na “IRC”. Kama madhara, shule hazikufunguliwa jumatatu hii. HABARI SOS Médias Burundi
Mashirika hayo mawili yanataka kuhudumu katika sekta ya elimu katika kambi za wakimbizi nchini Tanzania.Kawaida shirika la Save the children ndilo linahudumu katika sekta hiyo.
” Kwa wakati huu, mashirika mengine yaliachia nafasi shirika la Danish Refugee Council (RDC), shirika jingine la International Rescue Commitee linataka kupewa nafasi katika sekta ya elimu. Kwa hiyo mvutano unaripotiwa kati ya mashirika hayo mawili ya misaada. Tuna pia hofu kuhusiana na mishahara yetu”. anaeleza mwalimu mmoja katika kambi ya Nyarugusu.
Madhara ya mzozo huo ni shule kutofunguliwa jumatatu hii. Wanafunzi wamefukuzwa bila kuambiwa lini watarudi shuleni.
” Wanafunzi wetu wamekwenda sheleni lakini waalimu hawakuwepo. Waalimu wanaotoka nje ya kambi hawakuruhusiwa kuingia kambini. Kwa hiyo hatungetoa visomo wakati wenzetu wa Tanzania wakiwa wameshinda. Tunaomba swala hilo lijadiliwa kwa ngazi ya juu ili visomo katika awamu ya pili ya mwaka wa shule iweze kuendelea kama kawaida “, waalimu walielezea wakimbizi.
Kwenye kambi ya Nyarugusu, shule tano ziko chini ya uangalizi wa shirika la Save the children tangu miaka 7 iliyopita.
Katika kambi mbali mbali, urasibu wa mashirika ya misaada unahusisha HCR na serikali ya Tanzania. Wazazi wanaomba tatizo hilo liondolewe ili visomo visije kusimama kwa muda mrefu hususan katika darasa za mtihani na zile za kumalizia kidato.
Tatizo hilo linaripotiwa pia katika ya Nduta hata kama visomo bado kusimama.
Kambi hizo mbili zinajumulisha zaidi ya wakimbizi kutoka Burundi laki moja na elfu 26.
You might also like
Ituri: zaidi ya wananchi 200 waliuwawa na waasi katika kipindi cha miezi miwili
Tangu mwanzo wa mwaka 2023, hali ya usalama inazidi kuwa ya wasi wasi na kusikitisha katika mkoa wa Ituri karibu miaka miwili tangu kuanzisha serikali ya kijeshi. Wananchi wa kawaida
Nakivale (Uganda): Two NGOs celebrate Christmas for the vulnerable and albinos
Two humanitarian NGOs decided to join the vulnerable and albinos of the Nakivale camp to celebrate the end-of-year holidays starting with Christmas, a move welcomed by beneficiaries. INFO SOS Médias
Goma : angalau watoto 16 walifariki dunia kutokana na mazingira mabaya ndani ya kambi mpya ya wakimbizi wa ndani ya Majengo
Watoto wote 16 walifariki dunia katika kipindi cha chini ya wiki mbili. Kituo kinachowapa hifadhi wakimbizi hao wa vita kinapatikana katika kata ya Majengo tarafa ya Karisimbi. Ni katika mji
