Bujumbura: mripuko wa maradhi ya kipindupindu
Takriban watu 17 walipatikana na ugongwa wa Kipindupindu katika tarafa ya Kinama (kaskazini mwa jiji la biashara la Bujumbura) kulingana na waakazi. Wanahakikisha kuwa watu wawili tayari walifariki dunia. Ni visa vilivyoshuhudiwa tangu 30 disemba iliyopita. Waziri wa afya pamoja na muakilishi wa shirika la afya duniani OMS waliwasili jumapili hii katika tarafa hiyo ili kushuhudia hali hiyo. Mripuko wa ugonjwa wa kipindupindu ulitangazwa. HABARI SOS Médias Burundi
Waakazi wa tarafa ya Kinama wanafahamisha kuwa wanapata usumbufu wa kupata maji safi na vyoo vya viwango.
” Baadhi ya kata za karibu na tarafa ya Buterere wanashuhudia uchafu kutoka eneo la kata za Cibitoke na Mutakura ukimiminika katika maeneo ya tarafa hiyo. Ukosefu wa mifereji ni chanzo cha hali hiyo” wakaazi wanaeleza.
Jumapili iliyopita, ujumbe unaoongozwa na waziri wa afya na mjumbe wa shirika la afya duniani OMS (WHO) nchini Burundi waliwasili kushuhudia hali hiyo.
Waziri wa afya Daktari Sylvie Nzeyimana alitangaza kuwa eneo la kaskazini mwa jiji kuu la biashara linakabiliwa na mripuko wa visa vya ugonjwa wa kipindupindu . Alikiri kuwa visa 12 vya maradhi hayo vilipatikana wakiwemo watu 5 ambao tayari walipona na 7 wengine bado wanalazwa kwenye hospitali ya Prince Régent Charles (kati kati mwa jiji la Bujumbura)
Kupitia tangazo lililosomwa kwenye radio na Televisheni vya Burundi, alitangaza eneo la kaskazini mwa jiji la Bujumbura kuwa linakabiliwa mripuko wa ugonjwa huo wa kipindupindu.
Katika maeneo hayo, shughuli za kunyunyizia dawa majumba na vyoo katika familia zilizoshuhudia visa vya maradhi hayo ziliendeshwa jumapili hii na shirika la msalaba mwekundu nchini Burundi pamoja pia na ugaji wa maji safi
You might also like
Bujumbura : suspension of the celebration of the 4th anniversary of the CNL party
The Minister in charge of Home Affairs and Security has decided to suspend the double ceremony of the celebration of the 4th anniversary of the CNL party and the exchange
Kayanza : a health crisis due to the massive departure of doctors
Since the beginning of the year, the province of Kayanza, located in north Burundi, has been facing a wave of departures of doctors. No less than eleven practitioners have abandoned
Covid-19 : more than 200 cases detected
A strong spread of the Covid-19 pandemic has been reported in Bururi province in southern Burundi. At least 172 cases have been detected in this southern province of the country
