Ituri: angalau wananchi 28 waliuwawa katika mashambulizi ya waasi
Jumapili iliyopita, waasi wa kundi la silaha la CODECO (shirikisho kwa ajili ya maendeleo ya Kongo) walifanya mashambulizi katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa Ituri mashariki mwa DRC. Vyanzo vya ndani vinasema raia 28 waliuwawa, mali na madawa vikaibiwa. Mashirika ya kiraia ya ndani yanapongeza vikosi vya usalama kwa kuingilia kati mapema, lakini wanaomba taasisi hiyo kuongeza juhudi. HABARI SOS Médias Burundi
Mashambulizi hayo yalilenga vijiji na maeneo ya Bahema-kaskazini ndani ya wilaya ya Djugu, kwa mjibu wa mashahidi.
” Waasi wengi waliingia ndani ya soko la kijiji cha Nzengele tarafa ya Walendu-Binti. Walibomoa vibanda na maduka eneo hilo na kuwauwa watu 16″, mashahidi wanasema.
Wakati huo huo, waasi wengine wa kundi hilo walilenga ofisi ya uongozi wa Bahema-kaskazini eneo la Blukwa. Eneo hilo waliwauwa watu watano na kujeruhi mtu mwingine, pamoja na kuiba bidhaa. ilikuwa majira ya saa kumi na mbili , kwa mjibu wa vyanzo vyetu.
Kama vile hiyo haikutosha, kundi jingine lilielekea katika eneo la Walendu-Binti na Tatchi. Walishambulia parokia ya kanisa katoliki ya Drodro pamoja na hospitali kuu ya eneo hilo”, wakaazi wanalaani uporaji wa madawa na vifaa vya hospali.
Mashirika ya kiraia yanaripoti kuwa waasi walipita katika kijiji cha Largu ambako waliwauwa wananchi saba.
Matokeo ya mashambulizi ya jumapili ni watu 28 kuuwawa katika eneo la Bahema-kaskazini.
Mashambulizi hayo yalidaiwa kutekelezwa na CODECO wakati ambapo kundi hilo hivi karibuni lilishiriki katika mazungumzo ya Nairobi (Kenya) ambapo walisaini mkataba wa amani mkoa wa Ituri.
You might also like
Gitega : watuhumiwa watano wa mapenzi ya jinsia moja wameachiwa huru kwa jumla ya wale 24 wanaozuiliwa jela
Uamzi wa kuwaachilia huru umechukuwa jumatatu hii tarehe 20 machi, amethibitisha hayo mmoja kati ya mawakili waliotetea kundi hilo. Watano hao walioachiliwa huru walikuwa katika kundi la watu 24 wanaotuhumiwa
Gitega : a couple arrested for an alleged murder
A couple suspected of being involved in a murder that occurred in Songa, in the district and province of Gitega, was arrested by the police on Tuesday, February 11. INFO
Goma : several dead and injured in anti-Monusco demonstrations and against the EAC regional force
Several people were killed on Wednesday in the city of Goma, capital of North Kivu in the east of the DRC in demonstrations organized by a mystical-religious sect. According to
