Bubanza : kiongozi wa gereza kukamatwa na kupelekwa jela baada ya mfungwa kutoroka
Kiongozi wa gereza la Bubanza (magharibi mwa Burundi) Émile Nduwayo alisimamishwa jumatatu baada ya kuripoti mbele ya korti ya rufaa ya Bujumbura ( jiji la kibiashara). Faili hiyo ni baada ya mfungwa mmoja kutoroka. HABARI SOS Médias Burundi
Émile Nduwayezu kiongozi wa gereza la Bubanza alikuwa ametoa ruhsa ya kutoka nje ya gereza kwa habusu mmoja anayejulikana kwa jina maarufu Ngeni alipewa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela na faini ya franka za Burundi 555.555 za fidia katika mwaka wa 2013. Aliadhibiwa kwa kosa la mauwaji na wizi.
Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, muhalifu huyo aliomba ruhsa ya kwenda kuchukuwa pesa ndani ya taasisi moja ya fedha eneo hilo tarehe 27 februari iliyopita.
Alikuwa chini ya ulinzi wa askali polisi kwa jina la Evode Hakizimana. Tangu siku hiyo wawili hao hawakurudi kuonekana.
” Walichukuwa njia ya kuelekea Bujumbura badala ya kurudi jela. Walibadili hata nguo ili kijichanganya na raia wa kawaida. Polisi huyo kwa jina la Evode aliyemushindikiza Ngeni hadi sasa hapatikani kwenye simu” vyanzo karibu na faili hiyo vinathibitisha.
Baada ya kufahamu hali hiyo , mkuu wa gereza la Bubanza alitoa taarifa kwa mahakama ya mkoa huo kuhusu utoro huo siku moja baadaye.
Katika siku hiyo pia, aliwasilisha mashtaka dhidi ya Evode Hakizimana.
Uchunguzi uliendeshwa na uongozi wa juu ya idara ya magereza DGAP ndani ya gereza hilo.
Émile Nduwayo alisikilizwa katika mahakama kuu mbele ya korti ya rufaa ya Bujumbura tarehe 6 machi. Alipelekwa badaye katika gereza kuu la Bujumbura maarufu Mpimba kulingana na vyanzo vyetu.
About author
You might also like
Photo of the week : the Archbishop of Gitega calls on the CNDD-FDD and Burundian authorities to promote the respect for human rights
The ruling party in Burundi has organized a three-day prayer since Thursday in the political capital Gitega. It is the Archbishop of Gitega Monsignor Bonaventure Nahimana who read the opening
Bujumbura : Two police officers sentenced to pay fines for beating up a political party leader
It is the Ntahangwa Court in the north of the commercial city of Bujumbura that sentenced the two officers on Tuesday. Gabriel Banzawitonde, chairperson of the APDR party – the
Bunyoni case : the public prosecutor requested life jail for the former prime minister
The public prosecutor requested a life jail sentence for General Alain Guillaume Bunyoni and 30 years in prison for six other people prosecuted in the same case as him. The