Mutaho: aliyefanya mauwaji ya mrasibu wa kituo cha posta ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Mutaho: aliyefanya mauwaji ya mrasibu wa kituo cha posta ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Katika kesi ya mafumanio mbele ya chumba cha uhalifu cha mahakama kuu ya Gitega (mji mkuu wa kisiasa) jumamosi hii, Chadrack Irakoze (miaka 30) alihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la mauwaji ya kukusudia dhidi ya mrasibu mkuu wa kituo cha posta tarafani Mutaho Emmanuel Ndayizeye mwenye umri wa miaka 50. Muhanga aliuwawa kwa kupigwa risasi siku ya ijumaa akiwa ofisini mwake tarafani Mutaho mkoa wa Gitega (kati kati mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi

Dereva huyo na pia fundi mekanika mkaazi wa kijiji cha Bihororo tarafa ya Giheta( Gitega) alikiri kosa bila hata hivyo kueleza sababu za kufanya mauwaji hayo.

” Hakupora hata pesa. Hakika ni muuwaji aliyepewa jukumu la kumumalizia maisha muhanga”, alibaini mtu mmoja aliyesikikiza kesi hiyo.

Chadrack Irakoze alifahamisha kuwa alinunua silaha iliyofanya mauwaji hayo nchini jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo kwa ajili ya kijilinda.

Mwendeshamashtaka ya jamuhuri aliomba muhusika wa mauwaji hayo apewe adhabu ya kifungo cha maisha jela. Muhusika aliomba adhabu hiyo ipunguzwe.

Baada ya kutathmini majaji waliamuru apewe adhabu ya kifungo cha maisha jela.

Previous Rwanda-DRC: tuhuma za DRC kuwa Rwanda inafanya upelelezi dhidi yake ni ongezeko la vishawishi kwa wananchi kushambulia
Next Burundi: rais Neva anawatuliza watuhumiwa wanaofuatiliwa na ICC

You might also like

Security

Kakuma (Kenya) : a Burundian refugee killed

This Burundian was killed last Friday night. He reportedly fell into a group of armed bandits while returning from his carpentry, not far from the Kakuma refugee camp in northwestern

Security

Kanyaruchinya: eight deaths recorded in the IDP site

Eight people died between November 17 and 18, in the site of displaced persons who fled the fighting between the Congolese army and the M23 in Rutshuru territory to take

Security

Gitega: two unsolved murders in the districts of Gishubi and Mutaho

Two corpses were found in the districts of Gishubi and Mutaho, in the province of Gitega (central Burundi). It is the corpse of an ex-Fab (a retired soldier from the